Tangazo kwa wamiliki wote wa maeneo uwanja wa Ngongo.
Wamiliki wote wa maeneo ndani ya uwanja wa Nanenane Ngongo - Manispaa ya Lindi wanatakiwa kuanza kuyaandaa maeneo yao kwa ajili ya maonesho ya Nanenane kanda ya kusini 2019 ambayo hufanyika kuanzia tarehe 1-8 Agosti kila mwaka. Wamiliki wote wa vibanda vinavyozunguka uwanja wanatakiwa kumalizia ujenzi wa vibanda na wamiliki wa maeneo wanatakiwa kufanya usafi na kuandaa vipando. Tafadhali zingatia maelekezo haya kwani mwisho wa zoezi hili ni tarehe 15.06.2019 zaidi ya hapo wamiliki hao wa vibanda na maeneo watanyang'anywa maeneo hayo kwa mujibu wa makubaliano yaliyowekwa. Ukipata taarifa hii mjulishe na mwenzako.
Tunapenda kuwakumbusha wadau wote wa Maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kusini kuanza maaandalizi ya vipando vya muda mrefu na wakati kwenye maeneo yao katika viwanja vya maonyesho vya Ngongo.
Imetolewa na Kamati ya Uwanja, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi
Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi
Simu: 023-220-2098
Rununu:
Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz
Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.