• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

HALI YA MAAMBUKIZI YA VVU LINDI IKO JUU

Posted on: August 31st, 2022

Hali ya maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya UKIMWI mkoani Lindi imeonekana kuwa juu kutokana na uwiano wa takwimu za waathirika na idadi ya wakazi wa mkoa huu.

Akizungumzia kuhusu hali ya maambukizi kwa mkoa wa Lindi katika kikao cha maandalizi ya maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo kitaifa itafanyika mkoani Lindi mwanzoni mwa mwezi Disemba mwaka huu, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt.Kheri Kagya amesema idadi ya waathirika wa ugonjwa huo ni kubwa kuliko asilimia iliyopo kimkoa.

 “kwa takwimu za tafiti iliyofanyika mwaka 2016/17 ilibaini nchi yetu ina maambukizi ya asilimia 4.7%, mkoa wetu wa Lindi ulionekana kuwa na maambukizi ya asilimia 0.3% lakini katika mkoa huu tunao watu takribani 25,600 ambao ni wagonjwa wa Ukimwi na wanatumia dawa.”

“kwa hiyo mbali ya kuwa kiwango cha maambukizi kipo chini, lakini ukitafuta namba utakuta tunalo janga la Ukimwi katika Mkoa wetu”

Aidha Dkt. Kagya alitanabaisha kuwa hali hiyo imegusa pia rika ya watoto ambapo Dkt Kagya alisema kuwa, “….kati ya hao wapo zaidi ya 1,200 ambao ni watoto..”.

Dkt. Kagya ameelezea kuwa mkoa utatumia fursa iliyoipata ya kuwa mwenyeji wa maaadhimisho hayo kitaifa kueneza na kupeleka elimu kuhusu janga la Ukimwi kwa wananchi wa mkoa huo na watanzania kwa ujumla.

“Tumepata fursa hii ambayo itatusaidia kupeleka elimu zaidi ya Ukimwi kwa jamii yetu ili watu wetu waendelee kujikinga”.

Katika hatua nyingine Dkt. Kagya amesema wanatarajia kuendesha tafiti nyingine ambayo itatoa takwimu mpya za hali ya maambukizi kitaifa na kimkoa.

“Mwaka huu tutarajie kuna tafiti nyingine itafanyika ambayo itatupa tena hali halisi ya picha ya Ukimwi”

Kuelekea maadhimisho ya siku ya UKIMWI nchini, Dkt Kheri Kagya ameziomba taasisi nyingine ambazo zinajihusisha na utoaji wa huduma za afya kushiriki kwa pamoja katika kufanikisha zoezi hilo ambalo litasaidia kukumbusha uwepo wa janga hilo hapa nchini, na pia kutafakari na kuhamasishana kuhusu namna ya kujikinga, kujilinda na kujiepusha na ugonjwa huo na pia kuwapa usaidizi wa matibabu waathirika wa ugonjwa huo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.