• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

KAMATI YA BUNGE " LAAC" YAIPONGEZA SHULE YA LINDI SEKONDARI

Posted on: March 24th, 2023

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa wameipongeza Shule ya Lindi Sekondari kwa maendeleo makubwa kwenye ufaulu wa wanafunzi hasa kidato cha sita.

Pongezi hizo wamezitoa jana alhamisi walipoitembelea Shule hiyo Kwa ajili ya ukaguzi wa fedha zilizotolewa na Serikali kwa lengo la ukarabati na ujenzi wa madarasa mapya.

Akitoa pongezi hizo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Halima Mdee (Mbunge) amesema anaipongeza Shule na Walimu wote kwa kuutoa Mkoa wa Lindi kutoka mikoa ambayo ilikuwa haiheshimiki kwenye maendeleo ya elimu hapa nchini.

Mhe. Mdee ameongeza kuwa kwa mabadiliko haya makubwa ya elimu, mikakati iliyowekwa iendelezwe na kuendelea kuwapa  nguvu zaidi Walimu ili wajitume zaidi.

Awali akisoma taarifa ya Shule hiyo, Mkuu wa Shule Mwalimu Ramadhani Abdallah Divelle amesema kuwa Shule ya Lindi Sekondari kwa kidato cha sita ndani ya miaka mitatu mfululizo hali ya taaluma kwa kipindi hicho  imefanya vizuri Sana.

Kwa matokeo ya kidato cha sita mwaka 2020 Shule ilikuwa na jumla ya watahiniwa 204 Kati ya hao watahiniwa 27 walifaulu kwa daraja la kwanza, watahiniwa 130 walifaulu kwa daraja la Pili, watahiniwa 44 walifaulu kwa daraja la nne na watahiniwa 3 walifaulu kwa daraja la nne, ufaulu huu ukiwa ni asilimia 100.

Mwaka 2021, jumla ya watahiniwa walikuwa 173 na Kati ya hao 93 walifaulu kwa daraja la kwanza, 53 daraja la Pili, 27 daraja la tatu, ikiwa ni ufaulu wa asilimia 100.

Mwaka 2022 Shule ilikuwa na watahiniwa 232 na Kati ya hao 116 walifaulu kwa daraja la kwanza, 105 walifaulu kwa daraja la Pili na 11 walifaulu kwa daraja la tatu, ikiwa ni ufaulu wa asilimia 100.

 Akizungumza kama muhasisi wa mabadiliko hayo makubwa ya elimu Mkoani Lindi, Mkurugenzi wa Elimu kutoka OR-TAMISEMI Ndg. Vicent Kayombo amesema kuwa kabla ya kuwa mkurugenzi alikuwa Afisa Elimu wa Mkoa wa Lindi.

Ndg. Kayombo ameeleza kuwa akiwa Afisa Elimu wa Mkoa aliimarisha uongozi Bora na imara kwenye sekta ya elimu, kujenga upendo kwa Walimu na kushughulikia changamoto zao, kutoa motisha kwa Walimu pamoja, ku na kuandaa mpango wa Elimu wa Mkoa. Na Nchi nzima Mkoa wa Lindi pekee ulikuwa mpangokazi wa uboreshaji elimu.

Historia ya elimu ya Mkoa wa Lindi kwa miaka mingi imekuwa si ya kuridhisha. Ufaulu wa watahiniwa kwa Shule zote za msingi na Sekondari ulikuwa wa kiwango cha chini. Jitihada zilizofanywa na Viongozi wote wa Mkoa zimezaa matunda Bora ambayo yameufanya Mkoa wa Lindi kushika nafasi za kwanza na pili kwenye matokeo ya kitaifa ya kidato cha sita.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.