• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

KATIBU TAWALA BI. REHEMA MADENGE AKABIDHI OFISI KWA KATIBU TAWALA MPYA NDG. NGUSA SAMIKE

Posted on: August 10th, 2022

Aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bi. Rehema Madenge pamoja na Katibu Tawala wa Lindi wa sasa Ndg. Ngusa Samike Wamefanya makabidhiano ya Ofisi ya Katibu Tawala ya Lindi. Makabidhiano yamefanyika leo asubuhi katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Lindi.

Akikabidhi ofisi hiyo leo jumanne mbele ya Wakuu wa Idara pamoja na Waandishi wa Habari, Bi. Rehema amemkaribisha Ndg. Samike mkoani Lindi kwa kumueleza jiografia ya mkoa pamoja na uwepo wa fursa mbalimbali adhimu. Ameeleza kuwa Mkoa wa Lindi umejaa madini takribani yote ikiwemo dhahabu, graphite isipokuwa Tanzanite na almasi, lakini kwa kiasi kikubwa madini yanayopatikana ni aina ya jasi ambayo yanachimbwa sana Wilayani Kilwa maeneo ya Kilanjelanje kwaajili ya uzalishaji wa saruji, gypsum powder viwandani.

Pamoja na uwepo wa fursa nyingi za kiuchumi lakini bado matokeoya fursa hizo hayaakisi kwenye uchumi wa mkoa. “Lindi ni mkoa tajiri japo utajiri wake haujawa reflected sana na ndio kazi kubwa tunaendelea kufanya ili utajiri uliopo katika mkoa wa Lindi uonekane katika maisha ya watu……..kwa mfano kwenye korosho mpaka tunamaliza msimu tulifikia bilioni  142 lakini kwenye maisha ya wananchi huoni matokeo yake” ameeleza Bi. Madenge.

Bi. Madenge ameongeza kuwa ikiwa mkoa wa Lindi utatumia vizuri fursa za uchumi wa blue na vyanzo vya utalii kwa kutumia uwepo wa mbuga za wanyama, malikale , fukwe na bahari, Nyerere national park na serious game reserve inaweza kubadili hali ya maisha ya wananchi wa Lindi.

Kikubwa ambacho amesisitiza katika kuinua uchumi wa Lindi ni uimarishaji wa mawasiliano ambapo kwa sasa mawasiliano ya simu bado hayako vizuri kwenye maeneo mengi ya mkoa. Lakini pia miundombinu ya barabara za kuunganisha wilaya bado haiko vizuri hasa barabara za kwenda Liwale pamoja na maeneo ya Kilwa. Kufunguka kwa barabara nyingi za wilaya zitachochea maendeleo ya wananchi kwa kiasi kikubwa.  

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Lindi Ndg. Samike akimshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini amesema kuwa ametoka mkoa wenye ziwa lakini amekuja kwenye mkoa wenye bahari hivyo suala kubwa ni utumiaji wa fursa za bahari ikiwemo ufugaji wa samaki kwenye vizimba kama ambavyo mwanza wanafanya.

Ndg. Samike ameahidi kutoa ushirikiano ili kuendeleza yale yote mazuri ambayo Bi. Madenge aliyaanzisha lakini akisisitiza kusimamia vizuri masuala ya mapato, kupunguza vifo vya wamama na watoto, vifo vya watoto wachanga, kusimamia masuala ya lishe, fedha zote za barabara matokeo yaonekane. Pia ameahidi kushirikiana vizuri na Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye ni mwenyeji ili aweze kupata uzoefu Zaidi.

Ikumbukwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifanya mabadiliko ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mkoa nchi nzima mwishoni mwa mwezi Julai 2022 ambapo kwa upande wa Lindi aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa Bi. Rehema Madenge amehamishiwa Mkoa wa Dar es salaam na aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndg. Ngusa Samike amehamishiwa Mkoa wa Lindi.   

    

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.