• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Maandalizi ya Tamasha la Utamaduni la Jamii ya Lindi yaanza

Posted on: August 11th, 2018

Maandalizi ya Tamasha la Utamaduni wa Jamii ya Lindi yaanza

Wadau wa utamaduni katika mkoa wa Lindi wamefanya kikao chao cha kwanza cha maandalizi ya tamasha la utamaduni wa jamii ya Lindi litakalofanyika katika Kijiji cha Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.

Kikao hiki kiliongonzwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi na wajumbe wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Mkurugenzi Msaidizi wa Makumbusho ya Taifa, Bi. Agnes, Meneja wa TFS, Bi. Debora Mwakanosya, Wakuu wa Taasisi na Mashirika mbalimbali wa Mkoa wa Lindi, Mwenyekiti wa KAUJALI, Ndg. Abdalla Hanga, Maafisa Utamaduni, Viongozi wa vikundi vya Sanaa, na wataalam mbalimbali.

Bi Agnes aliwaeleza wadau mipango na namna tamasha hilo litakavyokuwa ambapo alisema kuwa tamasha litakuwa ni la siku nne. Siku ya kwanza kutakuwa na ufunguzi utakaoambatana na uzinduzi wa nyumba ya utamaduni wa jamii ya Lindi inayotarajiwa kujengwa katika eneo la makumbusho ya taifa.

Siku ya pili kutakuwa na kusomeana hadithi na simulizi mbalimbali kuhusiana na jamii za mkoa wa Lindi ambapo watu watapata nafasi kusikia kutoka kwa wazee mbalimbali watakaochaguliwa katika kusimulia historia za makabila na vitu mbalimbali. Siku ya tatu na ya nne viongozi na wadau mbalimbali watapata fursa ya kuzungumzia kuhusu maendeleo ya mkoa wa Lindi kuanzia mkoa ulipoanzishwa, ulipo na unapoelekea.

Naye Bi. Mwakanosya aliwaeleze wadau kuhusu fursa zilizopo katika utalii wa utamaduni na namna mkoa unavyotakiwa kujipanga kuonyesha utalii huo katika tamasha.

Mhe. Zambi aliwataka wajumbe wote kuhakikisha wanajipanga vizuri kuhakikisha tamasha hilo linafanyika kwa ubora unaostahili hasa ukichukulia mkoa wa Lindi ndio unaozindua kijiji kipya cha makumbusho ya taifa. Pia wakuu wa wilaya kuhakikisha wanakwenda kufanya uhamasishaji wa kutosha ili wananchi wengi waweze kutambua uwepo wa tamasha hilo ili wale watakaokuwa na uwezo waweze kushiriki.

Aidha, Mhe. Zambi amezitaka kamati zilizoundwa kukutana mara moja na kuanza kujipanga ni namna gani mkoa utalifanikisha tamasha hili kwani muda uliobakia ni mdogo sana. Wananchi wamehimizwa kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika tamasha hilo kwani licha ya kuonyesha masuala ya kiutamaduni pia watapata fursa ya kibiashara kwa kuonyesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza na kuziuza.

Tamasha la utamaduni wa jamii ya mkoa wa Lindi litafanyika tarehe 26 – 29 September, 2018 ambapo litaambatana na uzinduzi wa nyumba ya asili ya watu wa lindi itakayojengwa kijijini hapo. Kwa sasa kijiji cha makumbusho kinaanza kujengwa upya kwa kufuata ramani ya Tanzania, hivyo kila mkoa utatakiwa kuwa na nyumba ya asili ya mkoa husika kulingana na ramani ya Tanzania.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha maandalizi ya tamasha la utamaduni mkoa wa Lindi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.