• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE. NDEMANGA: WANALINDI TUJENGE UTAMADUNI WA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII.

Posted on: December 11th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Lindi, Mhe. Shaibu Ndemanga amewataka wananchi wa Lindi kujenga utamaduni wa kufanya utalii wa ndani katika maeneo mbalimbali ya kitalii ikiwemo maeneo ya fukwe za bahari na mbuga za wanyamapori zilizopo ndani ya mkoa wa Lindi.

Mhe. Ndemanga ameyasema hayo alipokuwa akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Lindi katika tamasha la utalii linalojulikana kama Kuchele Lindi Utalii Festival lililofanyika katika fukwe za bahari za kijiji cha Shuka kilichopo katika Halmashauri ya Mtama, mkoa wa Lindi.

“Niwatake wanakijiji wa Shuka na wanaLindi kwa kiujumla kujenga utamaduni wa kjufanya utalii wa ndani, kwa kutembelea vivutio mbalimbali za utalii kama utalii wa fukwe za bahari, mbuga za wanyama na maeneo mengine ya kihistoria. Sisi wenyewe tuwe na utamaduni wa kuvitembelea kwanza vivutio vyetu na tuvijue, mkoa wetu umejaaliwa kuwa na vivutio vingi vya kihistoria na ukisoma historia ya nchi hii ni mkoa wa Lindi pekee katika wilaya ya Kilwa ndo ulianza kuijua na kuitumia pesa yake” Mhe. Ndemanga.

“Ukienda kule Liwale unakutana na mbuga ya Selous, ukienda Nachingwea unakutana na historia kubwa ya ukombozi wa Afrika,nchi ya Afrika kusini na nchi nyingi za Afrika zimepata ukombozi kupitia Nachingwea hakuna viongozi waliodai uhuru ambao hawajakaa Nachingwea,kwaiyo tunawaomba wanaLindi tuchangamke kukaribisha wawekezaji ambao watatusaidia pia kukuza utalii katika mkoa wetu,na niwaambie tu serikali ya mkoa imekusudia kushirikiana na watu na sekta binafsi kukuza na kuutangaza utalii ndani ya mkoa wetu” Ameongeza.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amewahasa wananchi kutunza mazingira kwa kuacha kukata miti ovyo na kufanya usafi katika maeneo ya fukwe za bahari ili kuzidi kuvutia zaidi watalii katika maeneo yao.

“Lakini ndugu zangu wa Shuka na wanaLindi, utalii huu hauwezi kuwa mzuri kama hatujatunza mazingira yetu, twendeni tutunze mazingira yetu, tutunze uoto wa asili,tufanye usafi kwenye beach zetu ili wawekezaji hawa na watalii wafurahi wakiwa kwenye haya maeneo,tusikate miti hovyo, tusikate mikoko mana ndiyo inayopelekea kuzaliana kwa samaki. Na zaidi tujitahidi kuboresha na kulinda usalama wa watu na mali zao na sisi kama serikali tumejipanga zaidi kuboresha usalama katika mkoa wetu”

Naye, mkurugenzi mkuu wa Kuchele Beach Dkt. Bora Haule (PhD) amesema tamasha la kuchele utalii festival linalenga zaidi kutangaza fursa za utalii zilizopo ndani ya mkoa wa Lindi pamoja na fursa za uwekezaji katika utalii wa bahari hasa fukwe nzuri na safi zilizopo ndani ya mkoa.

“Uchumi wa buluu ni moja ya vipaumbele vya Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na tumekuwa na fursa za ufugaji wa majingoo bahari, kaa, ulimaji wa mwani ambazo ni fursa zinazopaswa kuchangamkiwa na wananchi wote. Aidha, uchumi wa buluu una fursa kubwa ya biashara, hivyo ni lazima tuhamasishe wananchi waweze kutumia fursa zinazopatikana humo ili waweze kuzalisha kwa wingi na kukuza vipato vyao” amesema Dkt. Bora.

     

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.