• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE. TELACK ATOA VYAKULA VYA SIKU KUU YA EID KWA WAFUNGWA NA WANAFUNZI

Posted on: April 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack jana alhamisi ametoa vyakula kwa ajili ya kusheherekea siku kuu ya Eid kwa wanafunzi wa bweni wa Shule ya Lindi Sekondari pamoja na wafungwa waliopo gereza la Lindi.

Akikabidhi vyakula hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemanga amesema kuwa Mhe. Zainab Telack ametoa mchele jumla kilogram 150, nyama kilogram 80 na mafuta Lita 10 kwa ajili ya taasisi  zote mbili.

Mhe. Ndemanga ameongeza kuwa vyakula hivi vimetolewa na Mkuu wa Mkoa ili kuwawezesha wanafunzi wa bweni zaidi ya 300 ambao wameshindwa kuungana na familia zao katika Sherehe za Eid. Pia amewakumbuka wafungwa waliopo gereza la Lindi ili wapate fursa ya kusheherekea siku kuu hiyo sambamba na wenzao waliopo mtaani.

Wakipokea vyakula hivyo, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Lindi Mwalimu. Ramadhan Abdallah Divelle amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuweza kutoa chakula hicho kwa wanafunzi wa Shule hiyo.

Akitoa shukrani zake kwa niaba ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Lindi, Mwanafunzi Noel Henny Lymo amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa upendo aliouonesha kwa wanafunzi wa Shule hiyo. Mwanafunzi Lymo ameongeza kuwa Mwenyezi Mungu ambariki Mkuu wa Mkoa kwa kutoa chakula katika siku muhimu kwa jamii ya kiislam sambamba na ndugu zao wakristo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Gereza la Lindi SP. Fadhili Juma Donile akipokea vyakula hivyo kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi La Magereza Mkoa wa Lindi ametoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa kwa kutoa msaada wa vyakula kwa wafungwa ambao utawapatia furaha sawasawa na wananchi wengine waliopo majumbani.

Hata hivyo, Baraza la Waislam, BAKWATA limetangaza jana alhamisi kutoandama kwa mwezi hivyo Siku kuu ya Eid haitokuwa Ijumaa na badala yake itakuwa Jumamosi ya tarehe 22 Aprili 2023.













ReplyForward






Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.