• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE. ZAMBI AWATAKA WANANCHI WA KIJIJI CHA MAKINDA KUTUNZA MIUNDOMBINU YA SHULE

Posted on: August 28th, 2017

MHE. ZAMBI AWATAKA WANANCHI WA KIJIJI CHA MAKINDA KUTUNZA MIUNDOMBINU YA SHULE

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewataka wananchi wa Kijiji cha Makinda kilichopo katika Kata ya Mangirikiti Wilayani Liwale kutunza miundombinu ya shule ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

Mhe. Zambi aliyesema hayo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ambapo katika shule ya msingi Makinda aliweka jiwe la msingi ujenzi wa madarasa 6, vyoo viwili vyenye matundu 10 na madawati 150. Ujenzi huu unafanyika chini ya mradi wa Lipa Kulingana na Mtokeo (P4R) na umegharimu shilingi 141,000,000.

Kabla ya ujenzi wa madarasa haya, shule ilikuwa na madarasa 2, ofisi moja ya walimu na nyumba moja ya mwalimu. Shule hii ina jumla ya wanafunzi 230 na walimu 3. Baada ya kuweka jiwe la msingi, Mhe. Zambi aliongea na wananchi wa Kijiji cha Makinda waliokuwa wamekusanyika shuleni ili kushuhudia uwekwaji wa jiwe la msingi.

“Nianze kwa kuwapongeza kwa kazi nzuri ya ujenzi wa miundombinu ya shule uliyofanyika chini ya mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (P4R), niwasihi wanafunzi, walimu na wananchi wote kwa ujumla kuhakikisha mnaitunza na kuilinda miundombinu ya shule ili iweze kudumu kwa muda mrefu, alisema Mhe. Zambi.

Katika mkutano huo Mhe. Zambi alipokea kero toka kwa wananchi ambapo wananchi walizungumzia tatizo la maji, nyumba za walimu, upungufu wa walimu na kwamba kijiji hakina zahanati. Wakijibu kero za wananchi Mhandisi wa maji, Mhandisi Adrew Kilembe alieleza kuwa mwezi Septemba, 2017 kisima kirefu kitaanza kuchimbwa chini ya ufadhili wa Godrill Company.

Kwa upande wa upungufu wa walimu, Afisa Elimu Msingi Wilaya, Ndg. Joseph Mhagama alieleza kuwa Halmashauri tayari imeshaomba kibali cha ajira ya walimu na watumishi wa kada nyingine ambapo walimu hao wakiletwa walimu 5 watapelekwa shule ya msingi Makinda. Kuhusu upungufu wa nyumba za walimu alieleza kuwa katika fedha za mradi zitakazo letwa halmashauri imepanga kujenga nyumba moja ya mwalimu. Vilevile alieleza kuwa jamii nayo inabidi ishiriki kwa kuanza kujenga boma ili halmashauri ije kumalizia.

Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Maulid Majala alisema kuwa kijiji kinapata huduma ya afya katika zahanati ya jirani ya kijiji cha Kipule ambayo ipo umbali wa kilomita 4. Ila halmashauri imepanga kuingiza kwenye bajeti ya 2018/2019 ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Makinda.

Katika ziara hii, Mhe. Zambi alitembelea shule ya sekondari RM Kawawa, Likongowele ambapo amekagua kuona kazi zinazofanywa na walimu. Pia ametembelea zahanati ya Kijiji cha Mbonde ambapo wananchi aliowakuta walimueleza kuwa wanaridhika na huduma wanayopatiwa na watumishi wa afya katika zahanati.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.