• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mhe. Zambi: Nendeni mkawe raia wema katika jamii

Posted on: December 10th, 2019

Mhe. Zambi: Nendeni mkawe raia wema katika jamii

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewataka wafungwa 129 waliochiwa kwa msamaha wa Rais kwenda kuwa raia wema katika jamii.

Zambi ameyasema hayo wakati akizungumza na raia 34 waliokuwa wafungwa katika gereza la wilaya ya Lindi alipokwenda kushuhudia utekelezaji wa agizo lililotolewa na Rais Magufuli la kutolewa gerezani kwa wafungwa waliopata msamaha bila kuwekewa vikwazo vyovyote.

Raia hao wamewatakiwa kwenda kushirikiana na jamii vizuri katika shughuli za maendeleo, japo inaweza kukatokea changamoto ya kuchelewa kukubalika katika jamii kutokana na matendo waliyoyafanya. Hivyo amewasihi kuwa wavumilivu na watulivu kwa kuionyesha jamii kuwa muda waliokaa gerezani wamejifunza mambo mengi na wamebadilika kuwa raia wema wanaoaminika.

Zambi amewaeleza kuwa wanatakiwa kumshukuru Rais Magufuli kwa msamaha aliowapatia na endapo watarudia kufanya makosa ambayo yatawarudisha gerezani wajue hatua kali zitachukuliwa dhidi yao kwani itakuwa ni kuutumia msamaha wa Rais vibaya.

“Baada ya Mhe. Rais Magufuli kuwaachia kwa msamaha, ni mategemeo yetu kuwa mnakwenda kuwa raia wema na mkajiepusha sana na mambo ambayo yamewasababishia kufika gerezani”, alisema Zambi.

Naye Mkuu wa magereza mkoa wa Lindi, SACP. Josephine Semwenda amewasihi wanajamii kuwapa ushirikiano raia hao kwani wakiwa gerezani walipata fursa ya kujifunza shughuli mbalimbali zikiwemo za kilimo, ufugaji, ujenzi na nyinginezo. Aidha, amesema kitendo cha kuwanyanyapaa na kuwatenga kinaweza wasababishi raia hao kurejea kwenye kufanya matukio ya kihalifu na kufungwa tena gerezani.

Mmoja ya wafungwa walioachiwa huru, ndg. Juma L. Magayane amemshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia msamaha, na ameahidi kwenda uraiani kutenda matendo mema kwani amebadilika kitabia. Pia alisema kuwa amejifunza mambo mengi alipokuwa gerezani hivyo ni malengo yake kwenda kushirikiana na jamii katika shughuli za maendeleo.

Katika mkoa wa Lindi wameachiwa wafungwa 129 ambapo kati ya hao gereza la Lindi wapo 34, gereza la Kilwa wapo 24, gereza la Nachingwea wapo 20, gereza la Ruangwa wapo 29, gereza la Liwale wapo 9 na gereza la Kingulungundwa wapo 13.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.