• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MKOA WA LINDI WAADHIMISHA MIAKA 59 YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA KUZINDUA OFISI ZA UHAMIAJI

Posted on: April 26th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack Leo tarehe 26 Aprili 2023 amezindua ofisi mpya ya Jeshi la Uhamiaji Mkoa wa Lindi, iliyojengwa Mtaa wa Msinjahili, Manispaa ya Lindi.

Uzinduzi huo umefanyika kwenye Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanzania zilizofanyika nje ya ofisi hiyo zikihudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Jeshi la Uhamiaji kutoka makao makuu na mikoa jirani, Viongozi wa Mkoa wa Lindi na Wilaya zake.

Akilipongeza Jeshi la Uhamiaji kwa kupata ofisi nzuri, Mhe. Telack amewaasa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo Mkoa wa Lindi kuuenzi na kuutunza Muungano wa Tanzania kwa kuilinda amani ambayo ni tunda la waasisi wa muungano.

Mhe. Telack amewasihi wananchi wa Mkoa wa Lindi kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama pindi wanapoona viashiria vya uvunjifu wa amani ikiwemo kuwafichua waovu.

Kwa upande wake, Kamishna wa Jeshi la Uhamiaji Novaita Edmund Mroso Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi hilo nchini Tanzania amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kulipatia  fedha Jeshi la Uhamiaji kwa ajili ya ujenzi wa Miradi mipya na kumalizia  miradi ambayo ilikwama kwa muda mrefu ikiwemo  jengo la ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Lindi.

Kamishna Mroso ametoa shukrani kwa uongozi wa Mkoa na wananchi wa Lindi Kwa kufanikisha Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanzania ambazo zimeenda sambamba na uzinduzi wa Jengo la ofisi ya Jeshi la Uhamiaji Mkoa wa Lindi.

Kamishna Mroso amesema kuwa jengo la ghorofa mbili lililozinduliwa kwenye Sherehe za Mkoa za Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack lilianza kujengwa mwaka wa fedha 2012/13 ambalo limegharimu takribani Tsh. Bilioni 2.2.

Kamishna Mroso ameongeza kuwa kukamilika kwa jengo la Ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Lindi ni hatua kubwa katika kufikia malengo ya miaka mingi ya kuwa na Ofisi ya Mkoa ambayo itawezesha utekelezaji wa majukumu kwa hari na ufanisi.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa, Mhe. Bakari Bwatamu ambaye ni Mwenyekiti wa Wilaya ya Lindi Mjini amesema kuwa Jeshi la Uhamiaji ni miongoni mwa majeshi yanayolinda amani ya wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Bwatamu ameendelea kwa kusema kuwa Jeshi la Uhamiaji ni walinzi wa mipaka ya kuingia nchini ambayo wamekuwa wakiilinda kwa uaminifu mkubwa. 

Mhe. Bwatamu amewaasa Askari wa Jeshi la Uhamiaji ambao wanaelekea kustaafu wawaelekeze vijana wanaowaacha kazini mbinu wanazotumia kuilinda amani ya nchi kwa pande zote mbili za Tanzania bara na Zanzibar.

Mkoa wa Lindi Leo Jumatano imehitimisha wiki ya kilele cha Maadhimisho ya Muungano wa Tanzania ambapo katika Sherehe zilizofanyika, Mhe. Telack ametoa zawadi za ushindi kwa wanafunzi watatu walioshiriki kwenye shindano la kuandika Insha inayohusu Miaka 59 ya Muungano wa Tanzania.



Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.