• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

PROGRAMU YA TAKUKURU RAFIKI YATATUA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU MIAKA 9 MKOANI LINDI.

Posted on: April 23rd, 2024

Ofisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa {TAKUKURU} Mkoa wa Lindi kupitia Programu ya TAKUKURU Rafiki imefanikiwa kutatua Kero ya ardhi iliodumu kwa muda wa takribani miaka tisa iliyokuwa inahusisha Eneo la Chuo cha Ufundi Stadi VETA na Ofisi ya Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Bi.Asha Kwariko katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Lindi, leo Machi 23, 2024 ambapo ameeleza kuwa kero hiyo imebainisha kuwa eneo ambalo chuo cha VETA waliomba kumilikishwa na Halmashauri ya Lindi ni dogo kulinganishwa na eneo walilolipa fidia wananchi ili waachie ardhi na kutokutekelezwa kwa mchakato wa kuonyeshwa mipaka ya eneo husika hivyo kuchelewesha mchakato wa Chuo cha VETA kumiliki ardhi.

"Kupitia majadiliano yaliyofanyika baina ya TAKUKURU Lindi, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi pamoja na wataalam wake kwa lengo la kupata majawabu, utatuzi wa kero hiyo ulipatikana ambapo VETA Lindi imeonyeshwa mipaka ya ardhi hiyo iliyoombwa kwa ajiri ya matumizi ya chuo hiko. Aidha, Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi ameifahamisha VETA Lindi kuwa eneo hilo ni mali yao na kwa sasa VETA imeanza mchakato wa umiliki wa ardhi hiyo kupitia ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa lindi na kuhusu ukubwa wa eneo walilopewa, majadiliano kati ya Taasisi hizi mbili chini ya uratibu wa TAKUKURU Lindi yanaendelea" ameeleza.

Aidha, TAKUKURU Lindi imeendelea na majukumu yake ya Uzuiaji wa Rushwa kwa kufanya Ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo katika kipindi cha mwezi Januari hadi Machi ambapo jumla ya miradi 12 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 7 kwenye sekta za Elimu, Maji, Kilimo, Uvuvi na Tamisemi na kubaini mapungufu katika miradi mitatu ya Elimu yenye jumla ya Shilingi Bilioni.  1,199,008,654.00 hivyo hatua mbalimbali zilichukuliwa ili kurekeebisha mapungufu hayo.

Vilevile, katika kipindi cha mwezi April hadi Juni 2024, TAKUKURU Lindi imejipanga kuendelea kutekeleza majukumu ya udhibiti vitendo vya Rushwa kwa kufanya ufatiliaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Mkoa wa Lindi, ufuatiliaji wa karibu wa ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri pamoja na ushirikishaji wa wananchi na wadau mbalimbali katika maeneo ya ushirikiano.

"Sambamba na hilo, tutaendelea kuchukua hatua stahiki kwa wale wote watakaobainika kufuja mali za umma, na kjwa kushirikiana na ofisi ya Taifa ya Mashtaka tutawafikisha mahakamani watuhumiwa wa vitendo vya Rushwa. Aidha, tutaendelea kutilia mkazo na kuongeza juhudi kwa kuhamasisha ushiriki wa wananchi kupitia nyenzo mbalimbali za uelimishajiumma, kufanya warsha na kuziendeleza klabu za kupambana na Rushwa mashuleni na vyuoni. Kupitia programu ya TAKUKURU Rafiki tutaendelea kuwashirikisha wananchi ambao ni wanufaika wa huduma zetu kutambua kero ambazo zikiachwa bila kupatiwa ufumbuzi zinaweza kusababisha mianya ya vitendo vya rushwa"

 

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.