• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mnada wa kwanza wa ufuta waonyesha mwanga

Posted on: June 19th, 2018

Mnada wa kwanza wa ufuta waonyesha mwanga

Mnada wa kwanza wa ufuta umeonyesha mwanga baada ya kilo ya ufuta kununuliwa kwa zaidi ya bei elekezi iliyowekwa na mkoa.

Haya yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake baada ya mnada wa kwanza wa ufuta kufanyika katika Kijiji cha Kitomanga Halmashauri ya Wilaya ya Lindi. Mnada huu umesimamiwa na Chama Kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao ambacho kinajumuisha wilaya ya Lindi na Kilwa.

Mhe. Zambi alisema kuwa mnada wa kwanza umeonyesha mafanikio kwani kilo moja ya ufuta imenunuliwa kwa sh. 2710 huku jumla ya kilo zilizoingizwa kwenye mnada ni 632,000 na zote zilinunuliwa. Bei elekezi ya ununuzi wa ya ufuta kwa kilo kwa msimu huu 2017/2018 ni sh. 1764 huku makato yakiwa ni sh. 103.

“Mnada huu wa kwanza umeanza vizuri kwa kilo moja ya ufuta kununuliwa kwa sh. 2710, ni matarajio ya mkoa kuwa bei hii itaendelea kupanda kwani kati ya kampuni 19 zilizojitokeza kwa ajili ya kununua ufuta katika mnada wa kwanza ni kampuni mbili tu ndizo zilizofanikiwa kununua ufuta wote ambazo ni Sunshine Commodities iliyonunua kilo 219,000 na The Agro Processing Africa Limited (TAPAL) iliyonunua kilo 413,000”.

“Kwa kuwa Ufuta bado unaendelea kukusanywa katika maeneo mbalimbali ndani ya Mkoa wa Lindi, niwaombe wakulima kuhakikisha wanauza ufuta wao kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Mkoa na sio kuuza ufuta kwa njia ya chomachoma ili waweze kunufaika na bei nzuri”, alisema Mhe. Zambi.

Aidha, Mhe. Zambi amewataka wananchi kuelewa kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa sio msimamizi wa biashara ya ufuta bali ni msimamizi wa kuhakikisha utaratibu wa ununuzi wa ufuta uliowekwa unatekelezwa. Hivyo msimamizi mkuu wa minada ya uuzwaji wa ufuta ni vyama vikuu vya ushirika ambapo kwa Mkoa wa Lindi kipo Chama Kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao na Chama Kikuu cha Ushirika cha RUNALI (kinajumuisha wilaya za Ruangwa, Nachingwe na Liwale).

Pia viongozi katika ngazi zote wametakiwa kuhakikisha wanasimamia mwongozo wa ununuzi wa zao la ufuta uliopitishwa na mkoa, na kuhakikisha wanadhibiti biashara ya chomachoma katika maeneo yao. Katika misimu iliyopita zao la ufuta limekuwa likinunuliwa kwa mfumo ambao sio rasmi tofauti na utaratibu unaotumika katika msimu huu.                                     

Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri uliweka utaratibu wa ununuzi wa ufuta ambapo kampuni yoyote inalazimika kufuuata ili iweze kuwa mnunuzi halali. Utaratibu huu unapatikana katika tovuti ya mkoa eneo la matangazo ambapo pia matangazo mbalimbali ya minada yatakuwa yakitolewa.

Baadhi ya wananchi wa Kitomanga na vijiji jirani

wakishuhudia mnada wa kwanza ukiendeshwa katika kijiji chao.

Vilevile Mhe. Zambi ametumia fursa hiyo kuwajulisha wanalindi kuwa mkoa utapokea Mwenge wa Uhuru Juni 20, 2018 katika Kijiji cha Madangwa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi ambapo utazunguka Halmashauri zote. Juni 26, 2018 Mwenge wa Uhuru utaondokea Halmashauri ya Manispaa katika uwanja wa ndege wa Kikwetu kuelekea Zanzibar. Mhe. Zambi amewasihi wananchi na viongozi wote kujitokeza kwa wingi katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utapita na katika maeneo ya mkesha.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • NDG. NGUSA SAMIKE AKABIDHI OFISI KWA BI. ZUWENA OMARY.

    March 20, 2023
  • KAMATI YA BUNGE YASISITIZA UJENZI WA MRADI WA BANDARI YA UVUVI UMALIZIKE KWA WAKATI

    March 19, 2023
  • BALOZI WA ZIMBABWE NCHINI TANZANIA ATEMBELEA MKOA WA LINDI.

    March 14, 2023
  • MAAFISA UGANI LINDI WAKABIDHIWA PIKIPIKI.

    March 13, 2023
  • tazama zote

Video

Zambi aagiza kampuni za kukopesha fedha zichukuliwe hatua.
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.