• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Uongozi wa Wilaya ya Ruangwa na kamati ya ujenzi wapongezwa kwa kusimamia ujenzi wa majengo ya Kituo cha Afya

Posted on: December 31st, 2017

Uongozi wa Wilaya ya Ruangwa na kamati ya ujenzi wapongezwa kwa kusimamia ujenzi wa majengo ya kituo cha afya.

Uongozi wa wilaya Ruangwa na kamati inayosimamia ujenzi wa majengo katika kituo cha afya Nkowe wamepongezwa na Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kwa kazi nzuri ya kusimamia ubora wa ujenzi wa majengo hayo.

Mhe. Majaliwa alitoa pongezi hizo wakati alipotembelea kituo cha afya Nkowe kukagua hatua ya ujenzi iliyofikiwa. Ambapo mpaka wakati anatembelea alikuta majengo yanayojengwa yakiwa katika hatua tofauti za umaliziaji na moja likiwa katika hatua ya lenta.

“Nimetembelea majengo yote yanayojengwa na kuridhishwa na kazi ambayo inafanyika, niwapongeze viongozi na kamati ya ujenzi kwa kazi nzuri ya usimamizi inayofanyika tena kwa kutumia mafundi wetu wa ndani. Kikubwa niwasihi muendelee kusimamia kuhakikisha fedha zinazotolewa kwa ajili ya ujenzi huu zinatumika vizuri na majengo yanajengwa kwa ubora unaotakiwa”, alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Mhe. Majaliwa aliwataka watumishi wa afya kufanya kazi kwa kuzingatia maadili yao ya kazi na kwamba serikali inaendelea kuzifanyia kazi changamoto walizonazo. Pia alimuagiza Mganga Mkuu wa Wilaya kuhakikisha dawa zinapatikana moda wote katika kituo. Vilevile aliwasihi wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano kwa kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao zikiwemo za ujenzi wa miundombinu.

Kituo cha afya Nkowe kimenufaika kwa kupata ruzuku kutoka serikali kuu kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ili kuimarisha huduma za uzazi na mtoto ambapo kilipokea shilingi 500,000,000. Fedha hizo ndizo zinazotumika katika ujenzi wa jengo la upasuaji, ujenzi wa nyumba ya mganga, ujenzi wa jengo la maabara, ujenzi wa wodi ya mama na mtoto, ujenzi wa kichomea taka, ujenzi wa jengo la uzazi, ujenzi wa visima viwili vya kuvunia maji ya mvua na ujenzi wa choo cha matundu manne.

Mpaka wakati Mhe. Mjaliwa alipotembelea fedha kiasi cha shilingi 232,473,050 ndizo ziizokuwa zimetumika kwa shughuli za ujenzi. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ruangwa, Ndg. Adrea Chezue alimuhakikishia Waziri Mkuu kuwa vifaa vyote vinavyohitajika baada ya ujenzi wa miundombinu kukamilika vipo hivyo wanachosubiri ni majengo kukamilika ili vifungwe.

Katika mkoa wa Lindi miradi hii inatekelezwa kwenye kituo cha afya Nyangamara (Halmashauri ya Lindi) ambapo tayari shilingi 384,316,500 na Kituo cha afya cha Kilwa Masoko (Wilaya ya Kilwa)ambapo tayari shilingi 270,000,000 zimeshatumika. Vituo hivi navyo vilipokea shilling 500,000,000 kila kimoja na kazi za ujenzi zinaendelea ambapo majengo yapo katika hatua mbalimbali za umaliziaji.

Miradi hii itakapokamilika wananchi watanufaika kwa kupata huduma hizi muhimu karibu na maeneo yao tofauti na awali ambapo walikuwa wanalazimika kwenda umbali mrefu ili kupata huduma hizi.  

Mhe. Majaliwa akitoa maelekezo baada ya kukagua 

ujenzi unaoendelea katika kituo cha afya Nkowe.

Jengo jipya la upasuaji katika Kituo cha Afya Nkowe

Nyumba mpya ya mganga katika Kituo cha Afya Nkowe

Kichomea taka kinachojengwa katika Kituo cha Afya Nkowe

Jengo la zamani la kuhifadhia maiti

Jengo jipya la kuhifadhia maiti

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.