Uongozi wa vyama vya ushirika mkoani Lindi umeonesha moyo wa huruma na mshikamano kwa jamii kwa kutoa msaada kwa wafungwa na mahabusu walioko katika gereza la mkoa huo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha ushirika RUNALI Ndugu Odas Mpunga alisema kuwa msaada huo umetolewa ikiwa sehemu ya nguzo ya saba ya ushirika .
Kwa upande wake Mrajisi Mkoa wa Lindi Ndugu Keneth Shemdoe amesema kutekeleza nguzo ya saba ni utaratibu wa kawaida ambao ushirika utaendelea kutoa huduma mbalimbali kwa jamii .
Shemdoe amesema kuwa hatua hiyo inalenga pia kupunguza mzigo kwa uongozi wa gereza katika kuhakikisha ustawi wa wahitaji walioko ndani ya mfumo wa haki jinai.
Aidha, Afande Christopher Yona Mwenda kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza amesema kuwa msaada huo wameupokea kwa furaha na kuushukuru uongozi wa vyama vya ushirika kwa moyo wa kujali. Walisema kuwa msaada huo ni wa kipekee na unaonesha mshikamano wa jamii na wale walioko kwenye changamoto ya kisheria.
Msaada uliotolewa umeelezwa kuwa ni pamoja na mahitaji ya kibinadamu kama sabuni, vyakula, na bidhaa za usafi, na umepokelewa kama ishara ya kujali utu wa wafungwa na mahabusu.
Uongozi wa vyama vya ushirika umetakiwa kuwa mfano kwa taasisi nyingine katika kuunga mkono juhudi za kijamii na kibinadamu.
@ushirika_tcdc
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi
Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi
Simu: 023-220-2098
Rununu:
Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz
Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.