• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Viongozi Tume ya Utumishi wa Umma wazungumza na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma Mkoani Lindi.

Posted on: November 2nd, 2017

Viongozi Tume ya Utumishi wa Umma wazungumza na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma Mkoani Lindi.

Viongozi wa Tume ya Utumishi wa Umma wamefanya ziara Mkoani Lindi kwa lengo la kukutana na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma na watumishi wa umma ili kuwaelezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Tume ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha kuhusu sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Akizungumza na viongozi wa taasisi za umma, Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bi. Salome Mollel alieleza kuwa tume ilianza kufanya kazi rasmi tarehe 7 January, 2004 ikiwa na kazi ya kufuatilia na kusimami uendeshaji wa shughuli za Rasilimali watu katika taasisi umma na kuhakikisha kuwa utumishi wa umma unaendeshwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.

Pia alieleza kuhusu majukumu ya tume kuwa ni pamoja na Kumshauri Rais kuhusu masuala ya utumishi wa umma kadri atakavyohitaji, Kutoa miongozo na kufuatilia uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu katika Utumishi wa Umma, Kupokea na kushughulikia rufaa za mashauri yaliyotolewa maamuzi na Mamlaka za Nidhamu, Kuwezesha, kufuatilia na kutathmini utendaji kazi wa watumishi wa umma wa ngazi mbalimbali ili uwe wa ufanisi na wenye kuzingatia matokeo.

Vilevile kuwaita Watendaji Wakuu kutoa maelezo kuhusu utendaji kazi usioridhisha pale Tume inapokuwa na ushahidi au malalamiko yanayohusu ukiukwaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu, Kuhakikisha kuwa Taratibu za Uendeshaji za Utumishi wa Umma wa makundi mbalimbali zinatayarishwa na kutumika ipasavyo na Kutekeleza majukumu mengineyo kwa mujibu wa Sheria mbalimbali zilizopo.

Bi. Mollel alielezea kuhusu muundo wa tume, majukumu ya waajiri, mamlaka za ajira na nidhamu katika utumishi wa umma na kwamba tume inasimamia masuala ya rasilimali watu katika utumishi wa umma.

Aidha, alieleza matarajio ya tume kuwa Waajiri, Mamlaka za Ajira na Nidhamu wanatekeleza maagizo ya Tume kwa wakati na kutoa taarifa ya utekelezaji wa maagizo hayo, Mamlaka za Ajira kuhakikisha kuwa ajira, upandishwaji vyeo na uthibitishwaji kazini unafanyika kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Utumishi wa Umma, Mamlaka za Nidhamu zinazingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo katika kushughulikia Mashauri ya Nidhamu ili haki iweze kutendeka.

“Wakuu wa Taasisi za Umma mnao wajibu wa kuhakikisha mnawasimamia kwa karibu watumishi walio chini yenu ili waweze kutimiza majukumu yao”, alisema Bi. Mollel. Huku akiwataka wakuu hao kuhakikisha wanafanyakazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu, miongozo na kuhakikisha wanafanyakazi kwa kuzingatia mipaka waliyowekewa.

Naye Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw.  Nyakimura Muhoji aliwasihi Maafisa Utumishi kuzingatia taratibu katika upandishaji wa vyeo hasa katika kigezo cha utendaji kazi mzuri. Pia aliwasihi kuacha tabia ya kutowasikiliza watumishi walio chini yao na kuwanyanyasa kwani tabia hiyo huwa ni kero kwa watumishi.

Vilevile aliwashauri Mhe. Meya, Wenyeviti wa Halmashauri, Naibu Meya na Manaibu Wenyeviti wa Halmashauri kutenga muda pamoja na madiwani ili waweze kupata elimu juu ya Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali ambayo itakuwa ikiwasaidia kwenye usimamizi wa shughuli mbalimbali za Hamashauri.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi alipokuwa akiongea na viongozi wa Tume aliwashukuru kwa maamuzi yao ya kufanya ziara katika mkoa wa Lindi. Pia aliwasihi kuwa watumishi wa Tume ya Utumishi wa Umma kuwa waadilifu kwani wanafanya kazi ya kuwasimamia viongozi na watumishi wa umma.

Mhe. Zambi alieleza kuwa katika kipindi hiki kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kiutendaji kwa watumishi wa umma kwani hata wananchi wamekuwa wakilisemea hilo. Hata hivyo bado kazi ya kuendelea kuwasimamia kuhakikisha watumishi ambao hawajabadilika wanabadilika.

Aidha, aliwaelezea fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo Mkoani Lindi zikiwemo uwekezaji mkubwa wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asili, Ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea, Madini ya Graphite na Gypsum, zao la Korosho, Ufuta na Utalii (Mbuga ya Selous). Pamoja na kuwakaribisha kuja Lindi, Mhe. Zambi amewaomba viongozi wa Tume ya Utumishi wa Umma kusaidia kuutangaza Mkoa wa Lindi kwani bado watu wanamtazamo wa zamani wakati sasa kuna mabadiliko makubwa.


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.