• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wafanyakazi watakiwa kujitathmini

Posted on: May 2nd, 2019

Wafanyakazi watakiwa kujitathmini

Wafanyakazi mkoani Lindi wametakiwa kutumia siku ya MEIMOSI kutathmini utendaji wao wa kazi ili kuona kama wanatimiza wajibu wao ipasavyo.

Wafanyakazi walielezwa hayo na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 1 Mei, 2019 ambayo kimkoa yalifanyika katika viwanja vya shule ya msingi mpilipili – manispaa ya Lindi.

Zambi aliwaeleza wafanyakazi kuwa siku ya meimosi inatoa fursa kwao kujitathmini kiutendaji, na kubaini vitu ambavyo vinaweza kuwa ni chanzo cha kuwakwamisha katika utendaji wao.

“Ni vema sote kwa pamoja tukajitafakari kama ni kweli tunatimiza wajibu wetu katika pande zote kwa maana ya waajiri na wafanyakazi kwani kila upande ukitimiza wajibu wake hakuna kitakachoshindikana”, alisema Zambi.

Wafanyakazi walielezwa kuwa serikali kwa upande wake inatambua changamoto walizonazo na tayari imeshaanza kuzifanyia kazi ikiwemo ya upandishaji madaraja na ulipaji wa madeni ya watumishi.

Pia aliwataka viongozi kuhakikisha wanaboresha ushirikiano na mshikamano baina yao na watumishi walio chini yao kwani kwa kufanya hivyo ndio kutasaidia kuondoa malalamikoa na manung’uniko kati yao wenyewe pamoja na watumishi wao.

Vilevile ametaka waajiri binafsi na wa taasisi zisizo za kiserikali kuzingatia haki na stahiki za wafanyakazi wao kwa kulipa maslai ya wafanyakazi wao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa, kwani kumekuwepo na malalamiko ya kutozingatia hilo.

Aidha, waajiri wote wametakiwa kuhakikisha michango ya watumishi inayokwenda kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii inapelekwa kwa wakati. Hili ni sambamba na kuhakikisha nyaraka zote muhimu za wastaafu zinakamilishwa kwa wakati ili mtumishi anapofikia ukomo mafao yake yapatikane kwa wakati.

Pia waajiri wote wametakiwa kusimamia vigezo vinavyotumika katika kumpata mfanyakazi hodari ili watu waache kupeana kwa kufuata nani mwaka jana kapata mwaka mwingine apate mwingine. Lengo hapa libaki ni kumpata mfanyakazi hodari, hivyo hata kama mtu amepata mara tatu na anasifa basi apate huyo huyo na si kupeana bila kuangalia vigezo.

Zambi amewataka watumishi kuwa na imani na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwani inashughulikia na inaendelea kusimamia haki na stahiki za watumishi. Hivyo amewasihi watumishi kuendelea kuchapa kazi kwa kila mmoja kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na maadili ya kazi yake.

Naye mratibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi (TUCTA) Bi. Fatma Chiwonga amewaomba waajiri kuwasaidia wastaafu kupata mafao yao kwa wakati kwani kumekuwepo na tatizo la kutokamilika kwa nyaraka zinazotakiwa kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kuyafuatilia katika mifuko husika.

Vilevile aliiomba serikali kuangalia uwezekano wa kupunguza makato ya kodi kwa watumishi kupitia mishahara ambayo kwa sasa wanakatwa asilimia 9 na kuomba ishuke mpaka asilimia 6 kwani wafanyakazi wengi wanaishi katika mazingira magumu.

Maadhimisho hayo yamebeba ujumbe wa "Tanzania ya uchumi wa kati inawezekana wakati wa mishahara na maslahi bora kwa wafanyakazi ni sasa".

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.