• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wanalindi Watakiwa kufanya kazi

Posted on: May 9th, 2019

Wanalindi watakiwa kufanyakazi

Wakazi wa mkoa wa Lindi hasa vijana wametakiwa kutumia muda wa kazi kwa kufanya kazi na si vinginevyo.

Kumekuwepo na tatizo la baadhi ya wakazi hasa vijana kutumia muda wa kazi kwa kucheza pool table, kunywa pombe na kufanya shughuli ambazo zimekatazwa kufanyika muda wa kazi.

Akizungumza na wakazi wa mtaa wa Nanyanje na Jangwani, wakati alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi aliwataka wakazi hao na mkoa mzima kutumia muda wa kazi kwa kufanya kazi na si vinginevyo.

“Wakati nikiwa njiani nimekuta vijana wanacheza pool table na wengine nimewakamata, niwasihi wananchi wote wa mkoa wa Lindi kuhakikisha mnafanya kazi na si kukaa kwenye vijiwe vya pombe, bangi, pool table na vingine kama hivyo wakati wa muda wa kazi”, alisema Zambi.

‘Kutokana na hili, niwaagize watendaji wote wa Kata, Mitaa na Vijiji kuhakikisha wanasimamia maelekezo yanayotolewa na serikali likiwemo na hili la vijana kutocheza pool muda wa kazi, kwani kwa kutofanya hivyo watachukuliwa hatua’, aliongeza Zambi.

Aidha, Zambi aliwataka viongozi wa wilaya kuhakikisha wanawasimami watendaji walio chini yao ili nao wahakikishe maagizo na maelekezo yanayotolewa na viongozi yanatekelezwa.

Pia wamiliki wote wa pool table wametakiwa kuzingatia na kutekeleza maelekezo ambayo yanatolewa na viongozi, kwani kwa kutofanya hivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga alisema kuwa maelekezo kuhusu agizo hilo walishayatoa sema kumekuwepo na baadhi ya wananchi ambao wamekuwa wakikaidi na pale ambapo wanakamatwa huchukuliwa hatua. Pia amemuhakikishia mkuu wa mkoa kuwa ataendelea kulisimamia agizo hilo huku akiwataka watendaji kutimiza wajibu wao wa kusimamia kwenye maeneo yao.

Kijana aliyekamatwa akicheza, Ismail Hassan ambaye ni mzaliwa wa mtaa wa Chikonji alisema kwa upande wake yeye hakujua kama kuna katazo lolote kwani walikuwa wakicheza pasipokuwa na katazo kutoka kwenye uongozi wa mtaa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.