• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Zambi awataka viongozi kuchukua hatua kuhusu tatizo la mimba za utotoni

Posted on: November 29th, 2019

Zambi awataka viongozi kuchukua hatua kuhusu tatizo la mimba za utotoni

Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi amewataka viongozi kuchukua hatua kuhusu tatizo la mimba za utotoni linaloukabili mkoa.

Zambi ameyasema hayo katika kikao cha kujadili tatizo la mimba za utotoni kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa. Kwa taarifa za mpaka Novemba, 2019 mkoa ulikuwa na jumla ya mimba 151 ambapo kati ya hizo 43 ni za shule ya msingi huku 108 zikiwa ni za sekondari.

Idadi hii ya mimba ni kubwa na ndiyo iliyosababisha uongozi wa mkoa kuitisha kikao hicho, kwa lengo la kujadili ukubwa wa tatizo ili kuweza kutoka na mikakati itakayosaidia kupunduza kama sio kumaliza kabisa tatizo hilo.

Zambi amewataka viongozi katika ngazi zote kwenye mkoa kuhakikisha licha ya kuwachukulia hatua wale wote wanaohusika na tatizo hili, waunde kamati za ulinzi wa mtoto kwa kila wilaya ambazo zitakuwa na wajibu wa kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu madhara ya mimba za utotoni pamoja na mambo mengine.

Pia maafisa elimu na maafisa ustawi wa jamii wameagizwa kusimamia uanzishwaji wa klabu rika katika shule na kwa shule ambazo zipo, ziimarishwe ili kusaidia utoaji wa elimu rika kwa wanafunzi wa shule husika.

Wazazi nao wametakiwa kuwa wa kwanza kusimamia mienendo ya watoto wao kuanzia nyumbani, shuleni na katika jamii badala ya kuwaachia walimu na jamii ndio ifanye kazi hiyo kitu ambacho kina sababisha watoto wengi kukosa maadili.

Zambi amesema kutokana na kupungua kwa maadili ya watoto ni vema sasa viongozi katika kila ngazi kuhakikisha vipindi vya dini shuleni vinarejeshwa na kusimamiwa ufundishwaji wake. Aidha, halmashauri zimetakiwa kuweka mkakati wa kuhakikisha zinafanya upimaji wa mimba wa mara kwa mara kwa wanafunzi hasa wanapokuwa wanakwenda likizo na wanaporejea.

Wajumbe katika kikao hicho wameonyesha kutokuwa na imani na mambo yanayofundishwa kwenye jando na unyago hivyo wameamua kabla ya unyago watoto wanaopelekwa wote waandikishwe kwa watendaji wa vijiji na mitaa, msimamizi wa watoto hao afahamike ili kumuona kama anafaa kwenda kukaa na watoto na kujua ni mambo gani watoto wanakwenda kufundishwa na kufuatilia ufundishwaji wake ili kama kutakuwa na mambo yasiyofaa yaweze kuzuiwa.

Aidha, imeshauriwa kufanyika uchambuzi katika kila wilaya ili kujua ni maeneo gani ambayo yanaongoza kwa tatizo la mimba za utotoni na kuchukua hatua madhubuti kwenye eneo husika badala ya kubaki na taarifa za jumla za wilaya na mkoa.

Waluu wa wilaya wameagizwa kwenda kufanya kikao kama hiki ambacho kitawashirikisha wajumbe katika wilaya na maafisa tarafa nao wafanye katoka tarafa, lengo likiwa ni kushusha maazimio ya kikao hadi ngazi za chini.

Wajumbe kwa pamoja walikubaliana kufanya vikao hivi mara mbili kwa mwaka ambapo watafanya tathmini ya hali ya mimba za utotoni pamoja na mambo mengine yanayohusu watoto.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.