Leo, Februari 13, 2026, Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Lindi imeendelea na ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Manispaa ya Lindi, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inatekelezwa ipasavyo mkoani humo.
Ziara hiyo iliongozwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Lindi, Ndg. Barnabas Y. Essau, akiambatana na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ndg. Juhudi Mgallah ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Mipango na Uratibu, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mhe. Victoria Mwanziva, wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa na wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Lindi, Ndg. Juma Mnwele, pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Manispaa.
Baada ya kutembelea na kukagua miradi tofauti ya maendeleo, Kamati imeridhishwa na maendeleo ya utekelezaji bora wa miradi hiyo, huku ikitoa pongezi kwa viongozi wa Wilaya kwa usimamizi thabiti na utekelezaji mzuri wa miradi hiyo kwa kuzingatia maelekezo ya Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Miradi iliyotembelewa ni pamoja Mradi wa Ujenzi wa shule mpya ya msingi kitomanga, mradi wa ujenzi wa Stand mpya Mitwero, Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Halmashauri Manispaa ya Lindi, Vilevile kamati imefanya ukaguzi wa jengo la kitega Uchumi (NHC) Pamoja na Barabara ya Bohari -NIDA.
Ukaguzi huo ni jitihada za kufuatilia kwa karibu maendeleo ya miradi inayoendelea kutekelezwa, ziara hiyo imefanyika kama sehemu ya tathmini ya mara kwa mara inayolenga kuimarisha uwazi na uwajibikaji, kuongeza kasi ya utekelezaji, na kuhakikisha miradi inaleta manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi wa Manispaa ya Lindi.
Kamati hiyo leo imehitimisha rasmi ziara yake iliyodumu kwa siku kadhaa, iliyohusisha Manispaa ya Lindi pamoja na halmashauri tano zilizopo ndani ya Mkoa wa Lindi.






Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi
Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi
Simu: 023-220-2098
Rununu:
Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz
Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.