• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mkoa Wa Lindi

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa Mkoa Wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

UZINDUZI RASMI WA MUONGOZO WA UWEKEZAJI MKOA WA LINDI

Sunday 11th, January 2026
@SEA VIEW BEACH RESORT - LINDI MUNICIPAL

“ Karibu katika mkoa wa Lindi, Asili ya Mjusi mkubwa na wa Kale kuliko mijusi yote mikubwa duniani na kituo sahihi kwa wawekezaji kufika na kutumia fursa zilizopo za Uwekezaji ”

Kazi iliyoko mbele yetu

Kazi kubwa tunayoitarajia hivi karibuni ni hatua ya kusambaza na kutangaza Mwongozo wa Uwekezaji Mkoani Lindi baada ya uzinduzi. Uzinduzi huu pamoja na mambo mengine unatarajiwa  kutaambatana na:-

  • Siku moja ya uwasilishaji, mjadala na kujenga mahusiano ya kibiashara miongoni mwa wadau/washiriki
  • Maonesho ya bidhaa zilizozalishwa na wajasiriamali katika mkoa wa Lindi (Katika  kipindi cha siku tatu)
  • Siku moja ya kutembelea maeneo yaliyobainishwa kuwa na fursa za uwekezaji mkoani Lindi.

Baada ya kukamilika kwa mpango huu, kinachotarajiwa ni kuwawezesha wote wenye nia ya kuja kuwekeza katika mkoa wa Lindi, kujitokeza na kuonesha nia, kuchagua kipaumbele/vipaumbele kulingana na mahitaji yao na uzoefu wao na kuamua kuwekeza kulingana na Sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa.

Mbinu za utekelezaji na hatua zilizopitiwa

Uongozi wa Mkoa wa Lindi unayo dhamira ya dhati ya kutekeleza mikakati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kukuza uchumi kupitia viwanda na kufikia uchumi wa kati nchini.

Kupitia ushauri wa kitaalamu wa Taasisi ya Utafiti wa Kichumi na Kijamii (Economic and Social Research Foundation- ESRF) kuanzia mwezi Mei, 2019 mkoa wa Lindi umekuwa katika mchakato wa kuandaa Mwongozo wa Uwekezaji (“Investment Guide”) ambao unatambua na kueleza kwa kina na ufasaha fursa zote za uwekezaji katika halmashauri zote sita za mkoa wa Lindi.

Kulingana na mpangilio uliotolewa na ESRF wakati  wa kuanza zoezi hilo, mchakato wa  kupata “INVESTMENT GUIDE”  hauna budi kupitia hatua saba muhimu za kitaalamu kama ifuatavyo:-

  •  Kikao cha mashauriano kati ya watafiti (ESRF) na Sekretarieti ya Mkoa,
  • Vikao vya mashauriano ya kupata habari kati ya watafiti (ESRF) na wadau katika ngazi ya halmashauri na kata mbili zilizoteuliwa katika kila halmashauri,
  • Utoaji na Ukusanyaji wa takwimu muhimu na habari nyingine za msingi zilizohitajika kuandaa Mwongozo wa Uwekezaji,
  • Utoaji wa taarifa za awali kutoka kwa watafiti (ESRF) na kujadiliwa katika kiiao cha pamoja kikihusisha Sekretarieti ya Mkoa na halmashauri zote sita,
  • Uchambuzi wa Takwimu na uingizaji wa takwimu hizo katika rasimu ya kwanza,
  • Uandaaji wa taarifa, uhariri na uhakiki wa usahihi wa taarifa husika,
  • Tafsiri ya Mwongozo katika lugha ya Kiswahili.

Kwa sasa mchakato umefikia hatua ya sita ambapo ESRF waliandaa na kuwasilisha rasimu ya Mwongozo katika Sekretarieti ya Mkoa kutoa fursa kwa wadau kuupitia na kuhakiki taarifa zilizomo ili kujiridhisha na usahihi kabla mwongozo huo haujazinduliwa rasmi.

Mkoa kwa kushirikiana na ESRF uliandaa na kuwa na kongamano la siku moja tarehe 29 Agosti, 2019 lililoshirikisha wadau mbalimbali kwa ajili ya uhakiki wa mwisho wa usahihi wa taarifa zilizomo. Maoni ya wadau yaliyotolewa yamefanyiwa kazi na kuingizwa katika chapisho la mwisho. ESRF na uongozi wa Mkoa wameafikiana uzinduzi rasmi ufanyike siku ya tarehe 27 Novemba, 2019

Muhtasari wa mwongozo kwa kifupi

Pamoja na mambo mengine chapisho la mwongozo linaweka bayana maeneo muhimu katika nyanja tatu zifuatazo:- 

  1. Vipaumbele vya uwekezaji katika ngazi ya mkoa ambavyo ni:- 
  • Viwanda vya kuchakata Chunvi hususani, Usindikaji, kuongeza thamani na ufungashaji.
  • Utengenezaji wa Chakula cha mifugo
  • Usindikaji wa mvinyo kutokana na mabibo.
  • Kiwanda cha kubangua korosho na vilainishi mitambo kutokana na maganda ya korosho
  • Kiwanda cha vifungashio

    2. Vipaumbele vya uwekezaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ni ambavyo ni:-

  • Uwekezaji unaolenga kukuza utalii kupitia fursa zilizopo za misitu/asili na fukwe,
  • Usindikaji wa korosho katika kuongeza thamani,
  • Vyuo vya ufundi stadi na ujuzi,
  • Viwanda vya kusindika mafuta ya kula,
  • Usindikaji wa mhogo,
  • Upandaji bustani za miche ya matunda,
  • Upasuaji mbao,
  • Vifaa vya ujenzi,
  • Uchimbaji na usindikaji wa madini,
  • Usindikaji wa mazao ya mboga na matunda,
  • Ufugaji wa nyuki na usindikaji wa mazao yake hususani asali
  • Viwanda vya maji ya kunywa/chupa
  • Kilimo cha umwagiliaji wa kibiashara hususani Mpunga na mbogamboga
  • Ufugaji wa samaki na viumbe wengine wa baharini.

    3. Sababu kumi na moja za kuwekeza katika mkoa wa Lindi zinabainishwa kuwa ni:-

  • Hali ya utangamano kisiasa na ulinzi wa uhakika na matukio machache ya uhalifu,

  • Uwingi wa mali asili ambazo zinatoa fursa kwa mapana katika kuongeza mnyororo wa thamani.
  • Uwepo wa ardhi ya kutosha na inayofaa kwa kilimo cha msimu, umwagiliaji, misitu na maendeleo ya viwanda.
  • Uwekezaji mkubwa wa miaka ya karibuni kwa miradi mikubwa katika maeneo jirani hususani Kiwanda cha Cement cha Dangote, uchimbaji wa gesi asilia na viwanda vinavyotarajiwa vya mbolea na uchimbaji wa madini ya Kinywe n.k.
  • Msukumo wa Serikali katika kuanzisha kituo maalumu cha uwekezaji (Special Economic Zone (SEZ) and a business park) karibu na eneo la uwekezaji wa kuchakata gesi asilia la Kikwetu.
  • Ukuaji wa soko la ndani ya mkoa- Kwa sasa mkoa unao wakazi wapatao 1, 082,346 kulinganisha na wakazi 787,624 waliokuwepo wakati wa Sensa ya Watu na makazi ya mwaka 2002 na wakazi 864,652 waliokuwepo wakati wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.
  • Kuimarika kwa miundombinu muhimu katika kukuza uchumi ikiwemo kukamilika kwa barabara ya lami kutoka Dar Es Salaam hadi Mtwara. Barabara inayopitia Lindi –Masasi na Mtambaswala katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji; ukarabati na upanuzi wa bandari ya Mtwara, kukamilika kwa bomba la usafirishaji mafuta kutoka Mtwara hadi Dar Es Salaa pamoja na ukarabati wa miundombinu ya kusambazia umeme.
  • Mipango madhubuti iliyopo ya kimkakati ya kupanua bandari ya Lindi pamoja na ujenzi wa Hospitali ya rufaa ya mkoa- Sokoine.
  • Vivutio vya asili vya utalii ikiwemo fukwe ambazo hazijachafuliwa, Mabaki ya magofu ya kale na mapango ya Kilwa, Hifadhi ya Selous n.k
  • Uwepo wa taasisi zisizokuwa za Kiserikali katika kuchochea maendeleo kuanzia za kimataifa na zile za ndani ya nchi.
  • Utashi wa kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii miongoni mwa Uongozi wa mkoa na Halmashauri katika kusaidia uanzishaji biashara mkoani, wakati Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) likiwa na dhamira ya dhati katika kukuza uchumi wa ndani miongoni mwa wakazi wa Lindi.

 “ Hautajutia kuamua kuwekeza katika mkoa wa Lindi.”

Washiriki binafsi, taasisi/mashirika watakaopenda kushiriki katika kongamano la uzinduzi wa Mwongozo wanaombwa kuonesha nia kwa kujaza fomu ya ushiriki inayopatikana kupitia website ya mkoa wa Lindi www.lindi.go.tz  na kutuma uthibitisho wa ushiriki kabla au ifikapo tarehe 25 November, 2019 kupitia barua pepe ps.ras@lindi.go.tz AU ras.lindi@tamisemi.go.tz nakala mipango@lindi.go.tz

Kupakua fomu ya ushiriki bofya hapa >>>>  FOMU YA USHIRIKI (REGISTRATION Form).pdf

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • LINDI: SIKU YA PILI YA UFUATILIAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 06, 2026
  • WAZIRI GWAJIMA: AIPONGEZA LINDI KWA KIKAO KAZI CHA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MKOA

    December 04, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII LINDI WATAKIWA KUWAJIBIKA

    December 04, 2025
  • RAS LINDI ATOA MAAGIZO 7 KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII.

    December 04, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.