• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Government Communication
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RAS LINDI ATOA MAAGIZO 7 KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII.

Posted on: December 4th, 2025

RAS LINDI ATOA MAAGIZO 7 KWA MAAFISA

MAENDELEO YA JAMII.


~Asisitiza Uwazi, Uwajibikaji na Utekelezaji.

Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri za Mkoa wa Lindi leo tarehe 04 Disemba 2025 wamekutana katika Kikao Kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Dockyard, Lindi Manispaa, chenye lengo la kujenga uwezo na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao katika sekta ya maendeleo ya Jamii.


Akizungumza katika kikao hicho, Mgeni Rasmi ambaye pia ni Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary, ameeleza kuwa serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Maafisa Maendeleo ya Jamii katika kuchochea maendeleo ya wananchi na kuboresha ustawi wa jamii. Ameeleza kuwa kazi wanazozifanya zimeendelea kuleta matokeo chanya, ingawa bado yapo maeneo yanayohitaji kuongezewa nguvu ili kuongeza tija na ufanisi katika ngazi zote.


Katika hotuba yake, Bi. Zuwena ametoa maagizo mahsusi kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii ili kuimarisha uwajibikaji, ufuatiliaji na utoaji wa huduma kwa wananchi. Ameelekeza kuimarishwa kwa ufuatiliaji wa vikundi vinavyodaiwa mikopo ya asilimia 10 kwa lengo la kusimamia marejesho, kuanzishwa kwa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi katika ngazi za kata, pamoja na kuimarishwa kwa mabaraza ya watoto yenye kufanya kazi kikamilifu kuanzia ngazi ya jamii.

Amesisitiza pia umuhimu wa utoaji endelevu wa elimu ya lishe, uundaji wa kamati za kupinga ukatili wa kijinsia katika ngazi za kata na wilaya pamoja na kuhakikisha vikao vya robo mwaka vinafanyika kwa mujibu wa mwongozo. Aidha, amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na miongozo ya utumishi wa umma, huku wakihamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika kuchangia na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Bi. Zuwena amesema hatua ya serikali kuunda Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum inalenga kuimarisha utoaji wa huduma kwa jamii na kuhakikisha wataalamu wa sekta hiyo wanatambulika na kuthaminiwa. 


Amewahimiza Maafisa Maendeleo ya Jamii kuunga mkono jitihada hizo kwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uwazi na kuzingatia dhamira ya serikali ya kuwatumikia wananchi.






Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • WAZIRI GWAJIMA: AIPONGEZA LINDI KWA KIKAO KAZI CHA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII MKOA

    December 04, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII LINDI WATAKIWA KUWAJIBIKA

    December 04, 2025
  • RAS LINDI ATOA MAAGIZO 7 KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII.

    December 04, 2025
  • NGOMA YA LIPUGA NGENDE

    December 04, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.