• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Bi. Madenge awataka wasimamizi wa uchaguzi kusimamia kiapo

Posted on: September 12th, 2019

Bi. Madenge awataka wasimamizi wa uchaguzi kusimamia kiapo

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Bi. Rehema Madenge amewataka wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa kuhakikisha wanasimamia uchaguzi kwa kuzingatia kiapo, sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

Bi. Madenge ameyasema hayo wakati wa zoezi la uapishaji wa wasimamizi hao lililofanyika katika ukumbi mdogo wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Lindi ambapo wasimamizi sita (6) wa uchaguzi kutoka halmashauri za mkoa wa Lindi waliapa kiapo mbele ya hakimu mkazi mfawidhi mkoa wa Lindi, Mhe. James Karayemaha na kushuhudiwa na baadhi ya watendaji wa ofisi ya mkuu wa mkoa.

Wasimamizi wametakiwa kutambua kuwa kiapo walicho apa sio cha utani kwani tayari wameshaweka ahadi mbele ya Mungu, serikali na wananchi hivyo endapo watakigeuka sio tu watapata adhabu kwa mujibu wa sheria bali hata kwa Mungu pia wataadhibiwa.

“Nimshukuru sana hakimu mkazi mfawidhi wa mkoa kwa ufafanuzi mzuri alioutoa kuhusu kiapo kwani kumekuwepo na uelewa mbovu wa kufikiri kuapa ni kitu sha masihara. Niwasihi wasimamizi wote kuhakikisha mnasimama katika kiapo chenu na kutoruhusu kutingishwa na mtu yeyote”, alisema Bi. Madenge.

Bi. Madenge amewataka wasimamizi hao kufanya kazi kwa ushirikiano na viongozi mbalimbali katika maeneo wanayotoka bila kuacha kusimamia misingi ya kiapo, sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi zilizopo ili uchaguzi utakaofanyika ufanyike kwa amani na utulivu.

Naye hakimu mkazi mfawidhi mkoa, Mhe. James Karayemaha amesema kuwa wasimamizi ni lazima watambue kuwa kazi wanayokwenda kuifanya ni nyeti sana kwani inahusu uchaguzi wa viongozi ambao watawaongoza wananchi kwa miaka mitano (5). Hivyo ni lazima watambue kuwa wao ndio chanzo cha utawala bora na chanzo cha maendeleo.

Mhe. Karayemaha amewasihi wasimamizi kutokuwa chanzo cha kuharibu uchaguzi kitu ambacho kitasababisha wao kupelekwa mahakamani kwa mujibu wa sheria na kusababisha serikali kuingia gharama za kuendesha kesi za uchaguzi katika mkoa na wao kuingia katika matatizo ambayo yanaweza wasababishia kufungwa.

Wasimamizi walioapishwa ni Ndg. Mohmoud Alli Kimbokota wa halamashauri ya wilaya ya Lindi, ndg. Michael Henze Maganga wa manispaa ya Lindi, ndg. Damas Mumwi wa halmashauri ya wilaya ya Liwale, ndg. Stephen Martin Pundile wa halmashauri ya wilaya ya Kilwa, ndg. Ally Mnunduma Adballah wa halmashauri ya wilaya ya Nachingwea na ndg. Selemani Amiri Mlope wa halmashauri ya wilaya ya Ruangwa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wasimamizi wameahidi kwenda kufanya kazi kwa kuzingatia kiapo, sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi ili uchaguzi uweze kufanyika kwa amani. Wote kwa ujumla wao wanatambua jukumu walilopewa ni zito hivyo wameomba ushirikiano kutoka kwa viongozi, wataalam na wananchi kwa ujumla ili waweze kulifanikisha kwa ufanisi.

Picha mbalimbali za uapisho ambapo kuanzia picha ya kwanza ni ndg. Stephen Martin Pundile wa halmashauri ya wilaya ya Kilwa, ndg. Mohmoud Alli Kimbokota (Lindi DC), ndg. Michael Henze Maganga (Lindi MC), ndg. Damas Mumwi (Liwale DC), ndg. Ally Mnunduma Adballah (Nachingwea DC) na ndg. ndg. Selemani Amiri Mlope (Ruangwa DC) na wengine ni wataalam kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakishuhudia zoezi la uapisho.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.