• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

BIL 296 ZATENGWA KUKAMILISHA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO NCHINI

Posted on: August 7th, 2025


- Mifugo laki 3 yatarajiwa kufikiwa na kuchanjwa Mikoa ya Lindi na Mtwara

Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 296 kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi la uchanjaji wa mifugo nchini, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kudhibiti magonjwa hatari yanayopunguza tija kwa mfugaji na kuathiri upatikanaji wa soko la kimataifa.


Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mifugo na Uvuvi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede, amesema serikali imepanga kufikia lengo la kuchanja asilimia 70 ya mifugo yote nchini ifikapo Oktoba 2025.


Kwa mujibu wa takwimu, jumla ya ng’ombe wanaokadiriwa kuwapo katika mikoa ya Lindi na Mtwara ni zaidi ya mifugo laki tatu na ambao nao wanatarajiwa kufikiwa na zoezi hilo, huku ikitarajiwa kuwa miongoni mwa mikoa inayotarajiwa kutekeleza kwa ufanisi zoezi hilo.

“Magonjwa yasipodhibitiwa huathiri kwa kiasi kikubwa thamani ya mifugo katika soko hasa la kimataifa. Serikali imeweka msukumo ili kuhakikisha zoezi hili linafanyika kwa ufanisi ili kufikia viwango vinavyokubalika kimataifa ili kuleta tija kwa mfugaji pamoja na kudhibiti tatizo la uwizi wa mifugo” alisema Dkt. Mhede.

Vilevile, Dkt. Mhede amesema kuwa serikali ya awamu ya sita inaendelea na mpango wake wa kuwawezesha wananchi kupitia sekta za kimkakati ikiwemo Kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuongeza msukumo ili kuhakikisha kuwa wananchi wote wanafikiwa na sekta hizi za kimageuzi, Katika upande wa uvuvi, serikali inaendelea kuwawezesha wavuvi wa ukanda wa pwani kwa kuwapatia boti za kisasa kupitia mikopo isiyo na riba, ili kuongeza tija katika shughuli zao na kuchochea uchumi wa buluu, na wakulima wakiendelea kunufaika na utolewaji wa pembejeo za kilimo bure.

Aidha, kupitia maadhimisho hayo, Dkt. Mhede amewakumbusha wananchi kuzingatia ulaji wa lishe bora, hasa protini zinazotokana na wanyama, huku akisisitiza matumizi ya bidhaa za mwani kwa afya na tiba, zikiwemo mafuta, unga na mbolea ya mwani pamoja na kuzitaka halmashauri kushirikiana na wataalamu kutoka idara za afya, lishe na maendeleo ya jamii ili kuhakikisha wananchi wananufaika na jitihada hizi za serikali katika kuboresha maisha yao.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YADHAMIRIA KUKOMESHA USAFIRISHAJI WA MAZAO GHAFI- DKT. JAFO

    August 08, 2025
  • DKT. JAFO AKOSHWA NA UBORA WA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KUSINI

    August 08, 2025
  • BIL 296 ZATENGWA KUKAMILISHA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO NCHINI

    August 07, 2025
  • TUJENGE TABIA YA KUTUMIA VYAKULA VYA ASILI NA MBEGU BORA

    August 06, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.