• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

CRDB yatoa msaada wa mbegu mkoani Lindi

Posted on: April 6th, 2020

CRDB yatoa msaada wa mbegu mkoani Lindi

Benki ya CRDB yatoa msaada wa mbegu za mahindi kwa wananchi waliokubwa na mafuriko.

Kama inavyofahamika kuwa mkoa wa Lindi ulipata tatizo la mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa zilizonyeesha na kusababisha kaya takribani 5,545 zenye watu 28,258 kupoteza makazi, chakula, mavazi na hata fedha. Wananchi hao katika moja ya msaada waliokuwa wakihitaji ilikuwa ni kupatiwa mbegu ili waweze kulima mazao mbalimbali ili waweze kulima na kujikimu na maisha yao.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Tully Mwambapa ambaye ni meneja mawasiliano amesema kuwa CRDB ilisikia kilio hicho cha wananchi kupitia kwa Mama Salma Kikwete (Mb) ambaye aliwafuata na kuwaeleza hitaji hilo. Benki kwa kuona umuhimu wake ikaona ni vema kuwasaidia wananchi.

“CRDB imetoa kilo elfu nne (tani 4) za mahindi zilizogharimu milioni ishirini (20) kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko waweze kulima mahindi yatakayowasaidia kwa chakula na hata biashara”, alisema Mwambapa.

Aidha, Mwambapa aliongeza kusema kuwa walijaribu kutafuta mbegu za aina nyingine za mazao lakini upatikanaji wake ukawa mgumu ndio maana wakaamua kuchukua mbegu za mahindi peke yake. Pia alisema kuwa CRDB ilishaanza kutoa msaada mafuriko yalipotokea kupitia tawi lake la Lindi ambapo walitoa magogoro, mashuka, nguo na nguo za kujisitiri za kina mama.

Mkuu wa mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi ameishukuru benki hiyo kwa kuendelea kutoka msaada kwa wananchi walioathirika na mafuriko kwani wamepoteza kila kitu. Msaada huu utawasaidia kuweza kuzalisha mahindi ambayo yatawasaidi kwa upande wa chakula na biashara kwa watakaofanikiwa kuzalisha vizuri.

Pia ameiomba benki kuendelea kutoa misaada mbalimbali pale panapokuwa na uhitaji na kuendelea kutoa mikopo kwa wananchi wa mkoa wa Lindi ambao wanataka kuwekeza au kufanya biashara. Kwani wapo wananchi wanataka kuyafanya hayo lakini wanakwama kwa kukosa mitaji.

Naye Mhe. Mama Salma Kikwete (Mb) amesema baada ya mafuriko kutokea aliwatembelea wananchi waliokubwa na mafuriko na kupata mahitaji yao ya aina mbalimbali likiwemo na hitaji la mbegu. CRDB alipowafuata kwa ajili ya kuwaomba msaada huo walimkubalia na kuahidi kulifanyia kazi.

Hivyo amewashukuru sana kwa kukubali ombi alilolitoa kwa niaba ya wananchi na kuleta mbegu hizo ambazo zitakuwa ni msaada mkubwa. Pia ameupongeza uongozi wa mkoa kwa kazi kubwa waliyoifanya wakati mafuriko yalipotokea na kuwaomba waendelee kuwa na ushirikiano huo hasa katika kuleta maendeleo katika mkoa wa Lindi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.