• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

DC MWANZIVA AKABIDHI VIFAA VYA MIL 179 UWEZESHAJI WAKULIMA WA MWANI LINDI.

Posted on: October 21st, 2025

DC MWANZIVA AKABIDHI VIFAA VYA MIL 179 UWEZESHAJI WAKULIMA WA MWANI LINDI.


Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Mh. Victoria Mwanziva, leo Oktoba 21, 2025, amekabidhi vifaa vya uwezeshaji wakulima wa zao la mwani katika kijiji cha Shuka, kata ya Navanga, Halmashauri ya Mtama vyenye thamani ya Shilingi Milioni 179. Ikiwa hafla hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi unaoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), kwa kushirikiana na Agriculture and Fisheries Development Program (AFDP).


Akizungumza katika hafla hiyo, Mratibu wa mradi huo, Ndugu Salim Mwijaga, alisema AFDP imekuwa ikitekeleza miradi ya kuwawezesha wananchi katika sekta za kilimo na uvuvi ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.


Kupitia ushirikiano huo, Serikali imefanikisha ugawaji wa vifaa mbalimbali kwa wakulima wa mwani katika vijiji vinne vya Shuka, Mmumbu, Mongomongo na Sudi.


Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na boti, chachacha, kamba kubwa na ndogo, kofia za usalama na glovu, ambavyo vinalenga kuboresha shughuli za kilimo cha mwani na kuongeza tija kwa wakulima.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya amesema Serikali itaendelea kuwezesha wakulima kupitia utoaji wa elimu, matumizi ya teknolojia za kisasa, pamoja na ushirikiano na wadau mbalimbali ili kukuza uzalishaji wa zao hilo muhimu na kuleta maendeleo ya kiuchumi nchini.


“Juhudi hizi zinazotekelezwa na Mh. Dkt. Samia suluhu, ambaye ni raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni moja ya utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi katika kukuza uchumi wa nchi, kupitia sekta hii ya uvuvi na uchumi wa blue ni sekta muhimu sana katika uchumi wa nchi yetu. Tukio la leo la kukabidhi vifaa na Boti vitavyotumika kulimia mwani katika halmasharui ya mtama ni sehemu ya mkakati wa serikali kuhakikisha uzalishaji wa zao la mwani unaongezeka. Hatua hii inalenga kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa vifaa na usafirishaji wa mwani kutoka shambani hadi maeneo ya kukaushia . Maboresho haya yatasaidia kuongeza tija na thamani ya zao la mwani, hivyo kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wakulima na jamii kiujumla” Amesema Mhe. Mwanziva.


Vifaa hivyo vitasaidia kuboresha shughuli za kilimo cha mwani kwa kurahisisha usafiri wa wakulima kufika mashambani, kuongeza usalama wakati wa kazi, na kupunguza gharama za uzalishaji. Zao la mwani limeendelea kuwa chanzo kikuu cha kipato kwa wananchi wengi wa eneo hilo.


Mmoja wa wakulima wa kijiji cha Shuka, Bi. Zuwena Sudi yusuph ameishukuru Serikali na wadau kwa msaada huo akisema:


“Tunaishukuru Serikali pamoja na wadau kwa kutupatia vifaa hivi. Awali tulikuwa tunapata shida ya usafiri kufika mashamba, sasa tumepata boti ambayo itarahisisha safari. Pia tulikuwa tunakosa kamba, lakini sasa tumepatiwa. Tunaishukuru sana Serikali kwa kutuona na kutuunga mkono.” Amesema Bi. Zuwena.


Kupitia kilimo cha mwani, wakulima wamekuwa wakipata kipato kinachowawezesha kukidhi mahitaji muhimu ya kijamii kama vile kugharamia elimu za watoto na mahitaji ya kila siku ya familia.



















Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WAPOKEA MAGARI MAPYA YA KISASA

    October 24, 2025
  • MKOA WA LINDI UPO SALAMA, WANANCHI WAKAPIGE KURA OKTOBA 29, 2025.

    October 24, 2025
  • RC LINDI AWAKABIDHI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MKOA WA LINDI MAGARI YA KISASA.

    October 24, 2025
  • DC MWANZIVA AKABIDHI VIFAA VYA MIL 179 UWEZESHAJI WAKULIMA WA MWANI LINDI.

    October 21, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.