• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Dkt. Bora abainisha sababu za akina mama kutojitokeza kupata matibabu ya fistula

Posted on: August 20th, 2019

DKT. BORA ABAINISHA SABABU ZA AKINAMAMA KUTOKUJITOKEZA KUPATA MATIBABU YA FISTULA.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Dkt. Bora Haule amebainisha sababu zinazosababisha akinamama ambao wamepata ugonjwa wa fistula kutokujitokeza kupata matibabu ya fistula katika uzinduzi wa kampeni ya matibabu ya fistula uliofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Lindi.

Dkt. Bora ametoa sababu hizo wakati akizindua mradi huo uliofadhiliwa na kampuni ya Equinor Tanzania ambao umelenga kutoa huduma za matibabu ya ugonjwa wa fistula bure kwa akinamama waathirika mkoani Lindi.

“Fistula ni ugonjwa unaomuondolea mwanamke staha na utu wake kwa kumsababishia kushindwa kuzuia haja ndogo na kubwa ambazo zote hutoka kwa kupitia njia ya uke”, alisema Dkt. Bora.

“Sababu zinazopelekea wanawake wengi kupata fistula ni pamoja na kuchelewa kupata huduma za afya wakati wa ujauzito hasa wakati wanapokaribia kujifungua,kupata mimba katika umri mdogo yaani mimba za utotoni na kukeketwa”, aliongeza Dkt. Bora.

Aidha, Dkt. Bora ameelezea sababu zinazopelekea wanawake wengi kushindwa kujitokeza wanapopata ugonjwa ambazo ni aibu, dhana potofu iliyopo ndani ya jamii ambayo imekua ikiamini kuwa mwanamke anaepata fistula ni yule ambaye ametembea na wanaume wengi wakati wa ujauzito. Pamoja na kushindwa kumudu gharama za matibabu ya fistula yanayojumuisha chakula, usafiri pamoja na gharama za matibabu yenyewe.

Pia amemshukuru mkurugenzi mkazi wa Equinor Tanzania Dkt. Mette Ottoey kwa kuchagua mkoa wa Lindi na kufadhili mradi wa matibabu hayo na kuongeza kuwa ofisi ya mkuu wa mkoa Lindi itahakikisha hospitali ya rufaa ya mkoa wa Lindi Sokoine inashirikiana na madktari kutoka hospitali ya CCBRT katika kufanikisha zoezi hilo la utoaji wa huduma ya matibabu ya fistula bure kwa wanawake wa mkoa wa Lindi.

Naye mkurugenzi mkazi wa Equinor Tanzania Dkt. Mette amesema anaamini kuwa jitihada wanazozifanya zitasaidia kuimarisha maisha ya wagonjwa walioathirika na ugonjwa wa fistula na zitawawezesha kuweza kurejea kwenye utekelezaji wa majukumu ya kila siku katika kujiletea maendeleo.

Mkurugenzi wa CCBRT, Brenda Msangi amesema wao wamejipanga kuhakikisha wataalam husika wanakuwepo katika kutoa huduma na kwamba wataendelea kuwajengea uwezo wataalam wa hospitali ili hata watakapoondoka huduma ya upasuaji dhidi ya fistula iendelee kutolewa.

 

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.