• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

DKT. JAFO AKOSHWA NA UBORA WA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KUSINI

Posted on: August 8th, 2025

MHE. DKT. JAFO AKOSHWA NA UBORA WA NANE NANE KANDA YA KUSINI NGONGO.

Mhe. Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Viwanda na Biashara  amefurahishwa na maandalizi na ubora wa viwanja vya maonesho ya Nane nane Kanda ya Kusini, vilivyopo Ngongo, Mkoani Lindi.


Pongezi hizo amezitoa akihutubia wananchi wakati wa kilele cha maonesho hayo yaliyofanyika tarehe 8 Agosti 2025, Mhe. Jafo ambaye alikuwa mgeni rasmi, amesifu kwa dhati juhudi za mikoa ya Lindi na Mtwara katika kuhakikisha viwanja hivyo vinakuwa vya kisasa, vyenye miundombinu bora ikiwemo barabara za lami, hali inayochochea ubora wa viwanja hivyo.

“Mmeweka alama ya kipekee kwa kuandaa viwanja vyenye hadhi na vigezo bora kwa maonesho haya. Hii ni hatua muhimu katika kutangaza fursa na kuhamasisha uendelezaji wa sekta ya kilimo na uchumi wa viwanda,” amesema Mhe. Jafo.


Katika hotuba yake, Mhe Jafo pia amezipongeza Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, akibainisha kuwa mikopo hiyo imekuwa kichocheo kikubwa katika kuimarisha biashara ndogondogo, shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Akizungumzia juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mhe. Jafo ameeleza kuwa zaidi ya shilingi bilioni 626 zimetolewa kwa ajili ya ruzuku ya pembejeo za kilimo, ambapo zaidi ya asilimia 85 ya pembejeo hizo zimeelekezwa katika mikoa ya Lindi na Mtwara, hususan kwa mazao ya kimkakati kama korosho.


Aidha, amewataka wananchi wa Kanda ya Kusini kutumia maarifa na teknolojia walizojifunza kupitia maonesho haya ya nane nane ili kuongeza tija katika uzalishaji, kuongeza kipato na kuchangia ustawi wa jamii.


Kauki mbiubya Maonesho ya Nane nane 2025 inasema “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025.”


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YADHAMIRIA KUKOMESHA USAFIRISHAJI WA MAZAO GHAFI- DKT. JAFO

    August 08, 2025
  • DKT. JAFO AKOSHWA NA UBORA WA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA KUSINI

    August 08, 2025
  • BIL 296 ZATENGWA KUKAMILISHA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO NCHINI

    August 07, 2025
  • TUJENGE TABIA YA KUTUMIA VYAKULA VYA ASILI NA MBEGU BORA

    August 06, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.