• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Government Communication
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

DKT. SHEKALAGHE AAGIZA HUDUMA KUANZA KUTOLEWA HOSPITALI MPYA YA RUFAA LINDI SOKOINE IFIKAPO JANUARI 1, 2026

Posted on: November 26th, 2025

DKT. SHEKALAGHE AAGIZA HUDUMA KUANZA KUTOLEWA HOSPITALI MPYA YA RUFAA LINDI SOKOINE IFIKAPO JANUARI 1, 2026 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, leo Novemba 26, 2025 amefanya ziara ya kikazi mkoani Lindi ili kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Hospitali Mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi – Sokoine, inayojengwa katika eneo la Mitwero, Manispaa ya Lindi.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Shekalaghe amesema kuwa lengo kuu ni kufuatilia utekelezaji wa mradi huo na kubaini changamoto zinazochelewesha kuanza kutolewa huduma, ili kuhakikisha zinapatiwa majibu ya haraka. 


Ameeleza kuwa wananchi wanasubiri kwa hamu kuanza kupata huduma katika majengo mapya ya kisasa. Dkt. Shekalaghe amesema kuwa ujenzi wa hospitali hiyo umefikia asilimia 98, ikiwa ni pamoja na usimikaji wa vifaa tiba muhimu kama CT-Scan na mashine za kisasa za X-ray. 


Amesisitiza kuwa ifikapo Januari 1, 2026, huduma zote lazima ziwe zimehamishiwa rasmi katika hospitali mpya ili wananchi waanze kunufaika na uwekezaji huo mkubwa wa Serikali. 


Aidha, Katibu Mkuu ametambua changamoto ya usafiri kwa watumishi wanaotakiwa kufika hospitalini mapema kila siku. 


Ameahidi kuwa Wizara italeta basi maalum kwa ajili ya watumishi ili kurahisisha usafiri na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma katika hospitali hiyo. Pia, Dkt. Shekalaghe amesisitiza umuhimu wa kusogezwa huduma muhimu za kijamii katika eneo linalozunguka hospitali hiyo, ikiwemo upatikanaji wa maji, umeme wa uhakika, maduka, maeneo ya chakula pamoja na makazi salama. 


Amesema hatua hizi zitaboresha mazingira kwa watumishi, wagonjwa na ndugu wanaowahudumia. Hata hivyo, amebainisha kuwa Wizara ya Afya itaendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa Mkoa wa Lindi na Hospitali ya Sokoine kuhakikisha hospitali hiyo mpya inakuwa kitovu cha huduma za kibingwa na bingwa bobezi. 


Lengo likiwa ni kupunguza rufaa zisizo za lazima kwenda mikoa mingine na hivyo kupunguza gharama kwa wananchi.



Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI, TAASISI ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI ZATAKIWA KUIMARISHA HUDUMA KWA WAJASIRIAMALI MKOANI LINDI

    November 27, 2025
  • UJENZI WA MADARAJA NA BARABARA KUSINI WAFIKIA 88%

    November 27, 2025
  • DKT. SHEKALAGHE AAGIZA HUDUMA KUANZA KUTOLEWA HOSPITALI MPYA YA RUFAA LINDI SOKOINE IFIKAPO JANUARI 1, 2026

    November 26, 2025
  • BODI YA KOROSHO TANZANIA YAWAPIGA MSASA MAAFISA BIASHARA MKOA WA LINDI.

    November 26, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.