• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

KUELEKEA MIAKA 71 YA SOKOINE RRH, MGANGA MKUU WA MKOA AZINDUA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA ITAKAYODUMU KWA SIKU 5.

Posted on: October 20th, 2025

KUELEKEA MIAKA 71 YA SOKOINE RRH, MGANGA MKUU WA MKOA AZINDUA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA ITAKAYODUMU KWA SIKU 5. 

Kuelekea Maadhimisho ya Miaka 71 tangu kuanzishwa kwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi Sokoine, Uongozi wa Hospitali hii imeandaa kambi maalumu ya Madaktari Bingwa kutoka hospitali mbalimbali za Rufaa kwa lengo la kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha utoaji wa huduma afya pamoja na kusogeza huduma za afya za kibingwa kwa wananchi. Akimuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Lindi katika uzinduzi wa kambi hiyo inayotarajiwa kutoa huduma kwa muda wa siku tano kuanzia leo Jumatatu ya Oktoba 20 hadi Ijumaa Oktoba 24, Katibu Tawala Msaidizi Afya Dkt. Kheri Kagya amewahimiza wananchi umuhimu wa kufatilia mwenendo wa afya zao na kugundua magonjwa yanayowakabili kabla hayajawa sugu mwilini. "Kuna kasumba mbaya miongoni mwetu hususani wanaume, ya kutokuja hospitali hadi tuwe tumezidiwa sana hii hupelekea ucheleweshwaji wa matibabu na kukomaza ugonjwa. Niwasihi wananchi tujenge utamaduni wa kuchunguza afya zetu na kuwahi katika vituo vya matibabu ili tupate huduma kwa wakati na tuendelee kulinda afya zetu na kuepuka kutumia gharama kubwa kwa ajiri ya matibabu" Aidha, Dkt. Kagya amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika Kambi ya Madaktari Bingwa ili kuweza kupata huduma za matibabu ya kibingwa na kusisitiza kuwa serikali imefanya uwekezaji mkubwa kuanzia kwenye miundombinu, vifaa tiba, madawa na wataalamu wa afya, lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya stahiki katika maeneo yao na kuwapunguzia gharama za kusafiri ili kupata huduma hizo. Bi. Salma Magota, mkazi wa kata ya Wailes ameshukuru ujio wa kambi hii kwani imewapunguzia mzigo wa kupata rufaa kwenda maeneo mengine. "Tumefurahi hospitali yetu imetukumbuka kwa kutuletea madaktari bingwa na kutuondolea gharama za kulipia ili kuonana nao, tuna imani kuwa changamoto zetu za afya zinaenda kupata tiba tukiwa hapahapa mkoani kwetu bila ya kusafiri" ameeleza. Kambi ya Madaktari Bingwa inajumuisha utoaji wa huduma za afya na matibabu ya kibingwa ya Magonjwa ya Mfumo wa Mkojo, Uzazi, Magonjwa ya Watoto, Magonjwa ya ndani, Mifupa, Ngozi, Kinywa na Meno na Upasuaji.






Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • MGANGA MFAWIDHI WA HOSPITALI YA RUFAA YA SOKOINE DKT. ALEXANDER MAKALLA AELEZEA HUDUMA ZA KIBINGWA ZINAZOTOLEWA KATIKA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA.

    October 20, 2025
  • KUELEKEA MIAKA 71 YA SOKOINE RRH, MGANGA MKUU WA MKOA AZINDUA KAMBI YA MADAKTARI BINGWA ITAKAYODUMU KWA SIKU 5.

    October 20, 2025
  • MIRADI YA MAENDELEO YA BIL 8 YAKAGULIWA LIWALE

    October 17, 2025
  • KILWA YANG’ARA NA MIRADI YA ZAIDI YA BIL 45

    October 18, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.