• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

LINDI MINING EXPO 2025 YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO – RC TELACK ATOA WITO WA KUCHANGAMKIA FURSA

Posted on: June 14th, 2025

Maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji Mkoa wa Lindi 2025 yamefungwa rasmi leo, tarehe 14 Juni 2025, wilayani Ruangwa, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, ameishukru Serikali, wadau na wananchi wote walioshiriki na kuwezesha mafanikio makubwa ya tukio hilo.

Katika salamu zake, Mhe. Telack ameeleza kuwa maonesho hayo yamekuwa daraja muhimu la kuwajengea uwezo wachimbaji wadogo na kutoa elimu ya kitaalamu kwa wadau wa sekta ya madini, huku akisisitiza dhamira ya Serikali ya Mkoa kuendelea kusimamia na kutangaza fursa zilizopo ili kukuza uchumi wa wananchi.


“Lindi ni Mkoa wa kukimbilia, si wa kutembea, tunahitaji kasi na mshikamano ili kila mmoja afaidi rasilimali tulizonazo, tutaendelea kutangaza fursa hizi kwa nguvu zote,” amesema Mhe. Telack.

Aidha, Maonesho hayo ya siku nne yaliyoanza tarehe 11 Juni 2025, yalifunguliwa na Mhe. Shaib Hassan Kaduara Waziri wa Maji Nishati na Madini kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa.

Kwa mujibu wa Mhe. Telack, zaidi ya washiriki 86 kutoka sekta ya umma na binafsi wameshiriki, huku maonesho hayo yakivuta zaidi ya wananchi 7,000 waliokuja kuona teknolojia, bidhaa na huduma mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini.

Katika kipindi cha maonesho, kulifanyika pia mafunzo ya kitaalamu yaliyolenga kuboresha uelewa na uwezo wa wachimbaji, huku yakiwa kichocheo cha mabadiliko chanya na washiriki wamepata ujuzi wa kipekee utakaowasaidia kuboresha shughuli zao kwa tija na usalama.

Mbali na hayo, Mhe. Telack ametumia jukwaa hilo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya madini na huduma za kijamii mkoani Lindi.

“Ninamshukuru sana Mhe. Rais kwa kutuamini na kuwekeza fedha nyingi katika Mkoa wetu, ikiwemo madaraja yaliyoharibiwa na mvua ambayo sasa wakandarasi wamelipwa na wanaendelea na kazi,” amesema Mhe. Telack.

Sambamba na hayo, ametoa pongezi kwa wadhamini wakuu wa maonesho akiwemo ELIANJE GENESIS CO. LTD, UVIWAMA, LINDI JUMBO, MINERAL ACCESS, PMBET na SI

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • RC TELACK AONGOZA KIKAO CHA WADAU WA KOROSHO, ATOA PONGEZI KWA MAAFISA UGANI

    July 03, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATANGAZA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE RUANGWA BAADA YA MIAKA 15 YA UONGOZI

    July 02, 2025
  • UJENZI WA CHUO KIKUU UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 65%, DKT. KIKWETE APONGEZA

    June 30, 2025
  • MHE. DKT. KIKWETEARIDHISHWA NA HATUA YA UJENZI TAWI LA UDSM LINDI

    June 30, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.