• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MAONYESHO YA MADINI LINDI 2025 YAZINDULIWA RASMI NA MHE. KADUARA

Posted on: June 11th, 2025

Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maoneesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Kaduara alisema thamani ya dhahabu imeendelea kupanda katika soko la dunia kutokana na athari za vita kati ya Urusi na Ukraine, ambako dhahabu inayozalishwa na Urusi imewekewa vikwazo kuingia katika masoko ya kimataifa.



"Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya 1996, pamoja na Sera ya Maendeleo ya Viwanda ya 1996–2020 na ile ya Viwanda Vidogo ya mwaka 2003, zipo kwenye mchakato wa kupitia upya kwa lengo la kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo ya kimkakati," alisema Kaduara.

Waziri huyo alibainisha kuwa miradi ya madini ni miongoni mwa miradi ya kimkakati nchini, ambayo inaendelea kufanyiwa tathmini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sera mpya itakayowezesha Watanzania kunufaika zaidi na sekta hiyo.

Lindi yajitokeza Kama Kitovu cha Madini Nchini

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack, alisema mkoa huo umebarikiwa kuwa na rasilimali kubwa za madini ambazo tayari zimeanza kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.


“Maonesho haya yanafungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Yanachochea uchumi wa eneo hili na kuongeza thamani ya madini tunayochimba,” alisema RC Telack.


Aliongeza kuwa maonesho ya awamu ya kwanza mwaka 2023 yalivutia wageni kutoka mataifa 14 na zaidi ya watu 6,000 walihudhuria, jambo lililoongeza hadhi ya Lindi kama eneo la kimkakati kwa shughuli za madini nchini.

“Kwa sasa tunaona ongezeko la wawekezaji, uboreshaji wa miundombinu na fursa za ajira, hali inayodhihirisha kuwa Lindi ni sehemu muhimu katika ajenda ya maendeleo ya taifa,” aliongeza.

Ongezeko la Wachimbaji na Teknolojia ya Uchimbaji

Kwa mujibu wa Mratibu wa Maonyesho hayo, Bw. Mwinjuma Mkungu, ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi mkoani Lindi, idadi ya wachimbaji imeongeka.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • RC TELACK AONGOZA MBIO ZA RIDHAA RUANGWA AISISITIZA UMUHIMU WA MAZOEZI,LINDI MINING EXPO

    June 12, 2025
  • "TUJENGE TABIA YA KUFANYA MAZOEZI MARA KWA MARA ILI KUIMARISHA AFYA ZETU" RC TELACK

    June 12, 2025
  • MAONYESHO YA MADINI LINDI 2025 YAZINDULIWA RASMI NA MHE. KADUARA

    June 11, 2025
  • MAONESHO YA MADINI NI FURSA KWA WANANCHI WA LINDI NA TANZANIA KWA UJUMLA- RC TELACK

    June 11, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.