MCHANGO WA MKOA WA LINDI WATAMBULIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2025 .
Ofisi ya Rais , Menejimenti ya Utumishi wa na Utawala Bora imekabidhi Cheti Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi kwa kutambua na kuthamani mchango wa Mkoa wa Lindi katika utoaji wa elimu na huduma kwenye maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma 2025.
Cheti hicho kimekabidhiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kwaniaba ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alitarajiwa kuwa mgeni rasmi wa maadhimiaho hayo.
Aidha, katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Omary amewapongeza wawakilishi wa watumishi ambao wameshiriki maadhimisho hayo yaliyoanza Juni 16 hadi 23, 2025 katika viwanja vya Chinangali Dodoma huku akiwasisitiza kwenda kuyafanyia kazi na kuwafahamisha wengine yale yote ambayo wamejifunza kutoka katika viwanja hivyo.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi
Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi
Simu: 023-220-2098
Rununu:
Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz
Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.