• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

MHE. TELACK AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

Posted on: November 6th, 2025

MHE. TELACK AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA.


Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack leo, Novemba 06, 2025 ameongoza kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe na Afua za Lishe Mkoa kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Juni 2025 kilichofanyika katika Ukumbi mkubwa wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.


Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhe. Telack amewataka viongozi na watendaji wote kuhakikisha wanasimamia ipasavyo utekelezaji wa shughuli za lishe katika maeneo yao sambamba na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu lishe bora ili kujenga jamii yenye afya.


“Lishe ni kipaumbele, Lishe ni chakula ni dawa, mwili wako ni kile unachokula. Hakikisheni fedha za lishe zinatoka kwa wakati na zinatumika kama ilivyokusudiwa. Kina baba na mama wajawazito wahimizwe kwenda kliniki pamoja ili kubaini mapema changamoto za upungufu wa damu na lishe na waweze kupata njia za kukabiliana nazo kwa pamoja ili kuimarisha afya ya mama kipindi cha ujauzito na mtoto anayetarajiwa kuzaliwa” amesisitiza.



Aidha, Mhe. Telack amesisitiza umuhimu wa kuimarisha sekta ya kilimo kupitia mashamba darasa kuanzia ngazi ya kijiji hadi kata, ili kutoa elimu sahihi kwa wananchi juu ya uzalishaji wa mazao ya chakula na bustani ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.


Vilevile,amewahimiza Maafisa Elimu kuhakikisha shule zote zinatenga maeneo ya wanafunzi kujifunzia kazi za mikono ikiwemo kilimo cha mazao mbalimbali ikiwemo ya chakula ili watoto wapate chakula cha mchana na kujifunza kazi za mikono na kueleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuandaa kizazi kinachowajibika na kinachothamini kilimo.


“Niwaombe sana kila mmoja kwenye nafasi yake asimamie vizuri ili tuweze kwenda sambamba. Kila mmoja akisimama vizuri tunaamini scorecard zetu zitakuwa kijani. Twende tukajenge lishe za wananchi wetu ili kupunguza sababu za wananchi kwenda hospitali mara kwa mara bila sababu za msingi,” ameeleza.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa Bi. Zuwena Omary amesisitiza uanzishwaji na ufuatiliaji wa mashamba darasa kuanzia ngazi za vijiji na kata ili kutoa fursa kwa wananchi kujifunza namna ya uzalishaji bora wa mazao ya chakula na bustani kwa tija ya kuongeza upatikanaji wa chakula na kuimarisha afya za wanajamii.


Afisa Lishe wa Mkoa Bi. Juliana Chikoti ameeleza kuwa kwa mwaka 2024/25 Mkoa umefanikiwa kutumia fedha kiasi cha shilingi milioni 311 kati ya milioni 376 zilizotengwa kwa ajiri ya kuratibu shughuki za huduma za lishe sawa na 86% na kubainisha changamoto kuu zinazokabili sekta hiyo ni pamoja na utoaji wa fedha za Lishe kwa wakati, ongezeko la watoto wanaozaliwa na uzito pungufu, upungufu wa unga wenye virutubisho, na idadi ndogo ya watoto wanaopata chakula shuleni.






Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • RATIBA YA MINADA YA KOROSHO MSIMU 2025 CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA RUNALI (RUANGWA, NACHINGWEA NA LIWALE)

    November 07, 2025
  • RATIBA YA MINADA YA KOROSHO MSIMU 2025/2026 CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA LINDI MWAMBAO

    November 07, 2025
  • MHE. TELACK AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    November 06, 2025
  • TAIFA LETU NI MOJA NA LINA NGUVU KULIKO MTU YEYOTE YULE

    November 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.