• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mhe. Zambi: Fanyeni kazi kwa uaminifu na uadilifu

Posted on: October 20th, 2018

Mhe. Zambi: Fanyeni kazi kwa uaminifu na uadilifu

Makatibu meneja wa vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) wametakiwa kuwa waaminifu na waadilifu katika kazi zao hasa kipindi hiki cha ununuzi wa korosho.

Wito huu umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi wakati akifunga kikao kazi cha makatibu meneja wa AMCOS ambacho kilifanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa.

Kikao hiki kilikuwa na lengo la kuwapa elimu ya pamoja juu ya namna mauzo ya korosho yatakavyoendeshwa msimu huu wa 2018/2019, namna bodi na mkoa ulivyojipanga, ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha majukumu yao. Pia mada mbalimbali ziliwasilishwa ambazo ni rushwa, bima ya afya, benki na watoa huduma za kifedha namna walivyojipanga, wakala wa vipimo, waendesha maghala pamoja na vyama vikuu.

Mhe. Zambi amewataka makatibu meneja kuhakikisha wanaelewa vizuri kuhusu bei dira na mjengeko wa bei. Ambapo amewataka kwanza waweze kutofautisha kwa kujua bei dira inapatikanaje na mjengeko wa bei unapatikanaje ili hata wakulima watakapokuwa wanawauliza waweze kutoa ufafanuzi mzuri.

“Kila mmoja wetu hapa amepata nakala ya mwongozo kutoka bodi ya korosho, hakikisheni mnakwenda kuusoma vizuri na mnatimiza yale yote yalimo ndani ya mwongozo huu”, alisema Mhe. Zambi. “Vilevile katika utendaji kazi wenu hakikisheni mnazingatia maelekezo yaliyotolewa wakati mada mbalimbali zikiwasilishwa”, aliongeza Mhe. Zambi.

Pia wametakiwa kuhakikisha korosho zote zinazoletwa na wakulima ni safi ili tatizo lililojitokeza mwaka jana kwa korosho kukutwa na mawe lisijirudie. Na kwa upande wa mizani wamesisitizwa kutohamisha mizani kuipeleka mashambani kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha mizani kuharibika na kusababisha kipimo kutokuwa sahihi.

Naye mwenyekiti wa chama kikuu cha RUNALI, Hassan Mpako alisema kuwa kikao kama hiki ni muhimu sana kufanyika kabla ya msimu wa mauzo ya korosho kuanza kwani makatibu meneja wa AMCOS ndio waandishi na watunza kumbukumbu. Hivyo elimu na maelekezo waliyoyapata yatasaidia katika kupunguza au kuondoa kabisa mapungufu yaliyojitokeza katika msimu uliopita.

Aidha, katika kikoa hicho, makatibu meneja waliapa kiapo cha ahadi ya uadilifu katika kuvitumikia vyama vyao vya msingi mbele ya Mhe. Lilian Rugarabamu, hakimu mkazi mahakama ya mkoa wa Lindi, huku wakishuhudiwa na viongozi mbalimbali walioongozwa na Mhe. Zambi.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.