• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

NI MUHIMU KUWATHAMINI WATOA HUDUMA ZA AFYA NGAZI YA JAMII- DKT GOWELLE

Posted on: September 6th, 2025


Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt.Otilia Gowelle amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii, hivyo wanapaswa kuthaminiwa.


Dkt. Gowelle amebainisha hayo leo Septemba 6, 2025 mjini Lindi wakati akizungumza katika Kikao cha Kamati ya Maandalizi kuelekea

hafla ya utoaji wa vyeti na kukabidhi vitendea Kazi kwa wahitimu wa mafunzo kwa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii itakayofanyika tarehe 8, Septemba, 2025.


Aidha, Dkt. Gowelle ameipongeza timu ya Kamati ya Maandalizi mazuri

chini ya Mganga Mkuu Mkoa wa Lindi Dkt. Kheri Kagya .


"Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wana umuhimu mkubwa, lazima sisi kama Serikali tuendelee kutambua mchango wao kwani wao ndio wanaotusaidia ngazi za chini kabisa kwenye jamii kwenye eneo la afya na kamati inafanya kazi nzuri kuelekea tukio hili muhimu na linapaswa liende kiutendaji zaidi," amesema.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Ernest Kyungu ameshukuru kwa ushirikiano mkubwa uliofanywa na Kamati ya Maandalizi.


Miongoni mwa watu walioshiriki Kikao hicho ni pamoja na timu kutoka Wizara ya Afya ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kinga Dkt.Otilia Gowelle, Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma Dkt. Ona Machangu Maafisa kutoka Wizara ya Afya na wawakilishi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Wengine ni Timu ya Uendeshaji Huduma za Afya Ngazi ya Mkoa (RHMT's), Timu Uendeshaji wa Huduma za Afya Ngazi ya Halmashauri (CHMT's) ,Uwakilishi kutoka Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi, Lindi, Uwakilishi kutoka Shule ya Sekondari Lindi pamoja na Uwakilishi kutoka Mkapa Foundation.

Kikao hicho kimefanyika katika Hospitali ya Sokoine Manispaa ya Lindi.


Wahitimu watatunukiwa vyeti baada ya kufuzu Mafunzo ya Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii waliyosoma katika vyuo vya afya kwa ufadhili wa Serikali kwa kipindi cha miezi sita (6) kupitia Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii uliozinduliwa na Makamu wa Rais Dkt.Philip Mpango Januari 31, 2024

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • NI MUHIMU KUWATHAMINI WATOA HUDUMA ZA AFYA NGAZI YA JAMII- DKT GOWELLE

    September 06, 2025
  • MAKUNDI MAALUM KUNUFAIKA NA MFUMO WA NeST- KIGAHE

    September 03, 2025
  • AAS MIPANGO NA URATIBU AFUNGUA MAFUNZO YA MFUMO WA MANUNUZI KWA WAJASIRIAMALI LINDI MANISPAA NA MTAMA DC.

    September 03, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA HAFLA YA UTOAJI VYETI NA VIFAA KWA WAHITIMU WA KOZI YA WATOA HUDUMA ZA AFYA NGAZI YA JAMII- WAJA

    September 07, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.