• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RAS LINDI ASISITIZA MATUMIZI YA TAUSI KATIKA KUBORESHA UKUSANYAJI WA MAPATO YA HALMASHAURI.

Posted on: January 24th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Jiri amewasisitiza maafisa biashara wa halmashauri za Mkoa wa Lindi kutumia mfumo wa Tausi ili kuboresha ukusanyaji wa mapato ya halmashauri kupitia kodi za leseni, kodi za majengo,kodi za mabanda, kodi za mabango na vibali vya ujenzi.


Katibu Tawala amesisitiza hayo wakati wa kufunga mafunzo ya siku tano yenye lengo la kutoa uelewa juu ya Maboresho ya Mfumo wa Tausi na Muse na utekelezaji wake katika ukusanyaji wa mapato na utoaji wa vibali kwa Maafisa biashara, Maafisa Ardhi na Wahandisi wa Halmashauri.

Akizungumza katika mafunzo hayo, katibu tawala ameeleza kuwa awali Halmashauri zimekua zikipata hasara nyingi na hoja zisizo za ulazima hivyo kupelekea kukosa makusanyo katika kodi ikiwemo kodi za mabanda,mabango, kodi za upandikishaji wa mabanda ya biashara, leseni za biashara, na vibali vya ujenzi na lazima kutokana na kukosa ujuzi na uelewa wa kutosha ya matumizi ya mfumo wa Tausi katika maeneo hayo.


"Mmejifunza kuzingatia na kufuata sheria, taratibu na miongozo zinazosimamia usimamizi,ukusanyaji wa mapato, uhasibu na uhandisi ili kuepuka hoja za kiukaguzi  na tunaamini maarifa haya yatachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha utendaji wa kazi na ukusanyaji wa mapato katika halmashauri zenu. Ni matarajio yetu kuwa mtaenda kufanya kazi kwa kuzingatia na kulingana na matarajio ya taasisi" Ameeleza.


Frank Kihunga, Mhandisi wa Halmashauri ya Ruangwa amesema mafunzo haya yamewapa mwanga wa matumizi ya vipengele vya mfumo wa Tausi ambavyo mwanzoni hawakua wakivitumia kutokana na kutokuwa na uelewa wa namna ya kuvifanyia kazi.


"Mafunzo haya ya maboresho ya mfumo wa Tausi yametupa uelewa wa matumizi ya vipengele ambavyo awali havikua vikitumika ikiwemo utoaji wa vibali vya ujenzi hivyo kuboresha mfumo mzima wa ukusanyaji wa mapato" ameeleza.


Naye, Bi. Ntuli Mwakyonde, Afisa Ardhi Halmashauri ya Kilwa ameeleza kuwa kupitia mafunzo haya wamejifunza namna ya uuzaji wa viwanja kupitia mfumo wa Tausi na namna ambavyo umerahisisha utendaji wa kazi.


"Kupitia mfumo huu mtu yoyote anaweza kupata huduma ya kuchagua na kununua kiwanja chake bila kuja ofisini hivyo kupunguza msongamano wa wananchi katika ofisi pamoja na urasimu" ameongeza Bi. Ntuli.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.