• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RC LINDI AWAKABIDHI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MKOA WA LINDI MAGARI YA KISASA.

Posted on: October 24th, 2025

RC LINDI AWAKABIDHI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MKOA WA LINDI MAGARI YA KISASA. 

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, Leo Oktoba 24, 2025, amekabidhi vitendea kazi kwa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Lindi, wakati wa zoezi la utayari uliohusisha na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Lindi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuimarisha utendaji wa kazi na kukabiliana na changamoto wakati wakati wa utekelezaji wa majukumu yao. Vitendea kazi vilivyokabidhiwa ni Magari ya ufuatiliaji na usimamizi pamoja na gari la wagonjwa la kisasa, Coman Car, Mtambo (Motor) Unaobeba Litre 5,000 za maji na povu la kemikali (chemical foam) ujazo wa lita 400 pamoja na gari dogo la ukaguzi. Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Telack amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika kuwajengea uwezo vyombo vya Ulinzi na Usalama ili viweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi na kutoa huduma bora kwa wananchi. 

“Haya ni matokeo ya dhamira ya Serikali kuhakikisha vyombo vya ulinzi na usalama vinakuwa na vitendea kazi vya kisasa. Ni jukumu letu sasa kuvithamini na kuvitumia kwa uadilifu katika kulinda usalama wa wananchi,” alisema Mhe. Telack. 

Aidha, aliwataka maafisa wa vyombo vya Ulinzi na Usalama kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kuimarika hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025. 

“Tuendelee kudumisha amani na kuhakikisha wananchi wanatekeleza haki zao za kupiga kura bila wasiwasi. Vyombo vyetu viwe mstari wa mbele katika kuilinda amani hii,” aliongeza. 


Kwa upande wake, Mrakibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Lindi, Joseph Mwasabeja ameishukuru Serikali kwa kuleta vifaa hivyo ambavyo vitasaidia kwa kiwango kikubwa kutatua changamoto zilizokuwa zinajitokea wakati wa utekelezaji wa majukumu yao. 

“Kupata vifaa hivi ni hatua kubwa kwetu. Vitatusaidia kuongeza kasi na ufanisi katika kukabiliana na matukio ya dharura na majanga, Kwa kiwango kikubwa sasa tumepata vifaa vingi vitaenda kutatua changamoto tulizokuwa tunakutana nazo” amesema Mwasabeja.










Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WAPOKEA MAGARI MAPYA YA KISASA

    October 24, 2025
  • MKOA WA LINDI UPO SALAMA, WANANCHI WAKAPIGE KURA OKTOBA 29, 2025.

    October 24, 2025
  • RC LINDI AWAKABIDHI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MKOA WA LINDI MAGARI YA KISASA.

    October 24, 2025
  • DC MWANZIVA AKABIDHI VIFAA VYA MIL 179 UWEZESHAJI WAKULIMA WA MWANI LINDI.

    October 21, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.