• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RC LINDI AZINDUA KAMPENI CHANJO YA POLIO

Posted on: April 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zainab Telack amezindua kampeni ya utoaji wa chanjo ya ugonjwa wa Polio kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 5, inayotarajiwa kufanyika katika mkoa wa Lindi kuanzia Aprili 24 hadi Mei 1.

Katika kikao hiko Mkuu wa Mkoa amewaomba viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini kutoa hamasa kwa waumini wao (wananchi) ili kuwafanya washiriki kikamilifu katika zoezi hili la utoaji wa chanjo kwa watoto ambalo linatarajiwa kufanyika nyumba hadi nyumba ili kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo hiyo.

“Niwatake wahudumu wa afya tuwe na  umoja na ushirikiano katika kulitekeleza zoezi hili la utoaji wa chanjo ya polio kwa watoto wetu, tukawe rahimu, tukawe na upendo katika kuwahudumia na kutoa chanjo kwa watoto wetu hawa” ameongeza Mhe. Telack.

Aidha, utoaji wa chanjo ya Polio unatarajiwa kuwafikia watoto wapatao 156,605 ndani ya mkoa wa Lindi ambapo Wakurugenzi na Maafisa wa Afya katika kila Halmashauri wametakiwa kuhakikisha kuwa fedha za chanjo zinatolewa kwa 100%.

Pia, katika uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha maeneo yao yanakuwa safi kwa kuyafanyia usafi na kufyeka nyasi ili kuharibu mazalia ya wadudu waenezao maradhi kama Mbu.

“Muwaambie watu wafyeke nyasi katika maeneo yao hasa katika msimu huu wa mvua, na sio kupulizia dawa mkawaambie madhara ya kupulizia dawa za kuua nyasi kuzunguka nyumba zao alafu wakaingia ndani kulala na watoto wao, wapeni elimu hawa wananchi na iwe marufuku kupulizia dawa hizi zenye sumu. Usafi kwenye barabara zetu na mitaro inayozunguka maeneo yetu isafishwe na hiyo kazi ifanyike kila Jumamosi katika wilaya zetu zote. Tunataka mashindano ya usafi kwa mikoa na sisi Lindi tuwepo na tuwe namba moja” Mhe. Telack.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.