• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RC LINDI, "MAAFISA LISHE TOENI ELIMU YA LISHE KWA JAMII"

Posted on: February 17th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewataka Maafisa Lishe wa Mkoa wa Lindi kutoa elimu ya lishe bora kwa kina mama wajawazito na wanaojifungua.

Mhe.Telack Akizungumza na wadau wa lishe Jana alhamisi kwenye kikao cha mkoa cha tathmini ya lishe amesema wataalam hao wasaidie kutoa elimu hiyo ili watoto wanaozaliwa wapate aina ya chakula kwa kuzingatia umri.  Ameongeza kuwa elimu ya msingi kwenye ukuaji wa mtoto inaanzia kwenye unyonyeshaji pindi tu mtoto anapozaliwa.

Mhe. Telack amesisitiza kuwa elimu hiyo itolewe Mkoa mzima ili wazazi waelewe vyakula bora vinavyosaidia ukuaji bora kwa mtoto. Ameongeza kuwa elimu hii itasaidia pia kupunguza tatizo la udumavu na utapiamlo kwa watoto.

Mhe. Telack ametoa wito kwa kina mama wajawazito na waliojifungua kuzingatia elimu ya lishe itakayosaidia uboreshaji wa afya ya mtoto, kujenga ubongo na mwisho kuwa na kizazi Chenye maamuzi sahihi.

Awali Akizungumza mbele ya wajumbe, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi Dkt. Khery Kagya amesema kuwa kwa sasa Mkoa wa Lindi unaendelea kusimamia na kuratibu programu za lishe kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali.

Dkt. Kagya ameongeza kuwa hali ya lishe kwa ujumla sio mbaya ambapo Kwa mujibu wa tafiti iliyofanyika 2018/19 kiwango cha udumavu kilikuwa 23.8 na kiwango Kwa mwaka 2020-22 kiwango cha udumavu ni asilimia 21.3. Takwimu hizi zinaufanya Mkoa wa Lindi kushika namba 4 kwa mikoa inayofanya vizuri katika kupambana na udumavu nchi nzima. Ameongeza kuwa lengo la Mkoa ni kumaliza kabisa tatizo la udumavu kwa watoto.

Akiwasilisha matokea ya hali ya lishe kwa tafiti zilizofanyika, Afisa lishe wa Mkoa Bi. Juliana Benjamin Chikoti amesema tatizo la udumavu na ukondefu linachangiwa kwa kiasi kikubwa unyonyesha mbovu wa watoto, Jambo ambapo linadumaza ukuaji wa ubongo wa mtoto na mwili kwa ujumla.

Kikao cha tathmini ya lishe Kimkoa hufanyika kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wa lishe ili kufanya tathmini ya hali ya lishe kwa Mkoa mzima na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazobainishwa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.