• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

RUANGWA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI MIAKA 6 MFULULIZO

Posted on: June 18th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omari, ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kupata Hati Safi kwa miaka sita mfululizo katika ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ametoa pongezi hizo leo tarehe 17 Juni, 2025 katika kikao maalumu cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Ruangwa kwa ajili ya kuchambua na kujadili taarifa ya CAG ya mwaka wa fedha 2023/2024.


Kikao hicho kimehusisha Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri hiyo, Wakuu wa Idara na Vitengo (CMT), Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Wakaguzi kutoka Ofisi ya CAG Mkoa wa Lindi, Katibu wa Waziri Mkuu, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Katibu Tawala wa Wilaya pamoja na wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa wa Lindi.

Aidha, akiwasilisha salamu za Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, Bi. Zuwena amesema kupata Hati Safi kwa miaka mitano mfululizo ni ishara ya utendaji bora, uwajibikaji wa hali ya juu na usimamizi mzuri wa rasilimali za umma.

“Niwapongeze kwa dhati kwa kupata Hati Safi kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo, hii siyo kazi rahisi bali ni matokeo ya mshikamano, uadilifu na kujituma kwa viongozi wa kisiasa na wataalamu wa Halmashauri ya Ruangwa,” amesema Bi. Omari

Vile vile, ameongeza kuwa ufanisi huo unapaswa kuwa mfano kwa Halmashauri nyingine ndani ya Mkoa na kuwataka viongozi waendelee kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mapendekezo ya CAG ili kuimarisha zaidi mifumo ya kifedha na kiutawala.

Sambamba na hayo,  Bi. Zuwena ameagiza hoja zote zinazoweza kufutwa zifanyiwe kazi na ili zifutwe mara moja maana zipo ndani ya uwezo wa Halmashauri.


Baraza hilo maalumu ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ambapo Madiwani hukutana kuchambua taarifa ya ukaguzi wa CAG kwa lengo la kuweka mikakati ya maboresho na kuongeza uwazi katika matumizi ya fedha za umma.


Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • RC TELACK AONGOZA KIKAO CHA WADAU WA KOROSHO, ATOA PONGEZI KWA MAAFISA UGANI

    July 03, 2025
  • WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATANGAZA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE RUANGWA BAADA YA MIAKA 15 YA UONGOZI

    July 02, 2025
  • UJENZI WA CHUO KIKUU UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 65%, DKT. KIKWETE APONGEZA

    June 30, 2025
  • MHE. DKT. KIKWETEARIDHISHWA NA HATUA YA UJENZI TAWI LA UDSM LINDI

    June 30, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.