• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

SERIKALI YATAMBUA MCHANGO WA WATOA HUDUMA NGAZI YA JAMII.

Posted on: March 15th, 2024

Watoa Huduma ngazi ya Jamii wametakiwa kuendelea kufanya kazi nzuri ya kuelimisha jamii kuhusu masuala mazima ya afya ili kuzidi kutoa chachu kwa wanajamii kuhudhuria katika vituo vya afya na hospitali wanapougua au kupata dalili za hatari pamoja na kupata elimu mtambuka.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu wa Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, Mkoa wa Lindi yenge lengo la kukagua hali ya upatikanaji wa huduma za afya kwa wanajamii pamoja na utekelezaji wa miradi ya afya katika wilaya hiyo ambapo katika ziara hiyo Dkt. Magembe alitembelea katika Kituo cha Afya cha Liwale Mji na kujionea mchango mkubwa unaofanywa na Watoa Huduma za Afya ngazi za Jamii katika kutoa elimu inayowahamisha wananchi hususani akina mama wajawazito kuhudhuria kliniki, kuhakikisha wanajifungua katika vituo vya afya na kutoa elimu ya unyonyeshaji pamoja na dalili za hatari zinazoweza kumpata mtoto na mama baada ya kujifungua.

Aidha, Dkt. Magembe ameeleza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya inatambua mchango wa watoa huduma  kwa jamii kama kiunganishi baina ya wananchi na huduma za afya hivyo kuja na mpango maalumu wa  kuwapatia elimu na ujuzi watoa huduma ngazi ya jamii ili kuweza kuwarasimisha.

"Serikali ya awamu ya sita imeandaa programu maalumu inayoitwa A Coordinated Intergrated Program of Community Health Workers ambayo inaenda kuwarasimisha watoa huduma ngazi ya jamii kwa kutangaza nafasi za kazi za wahudumu kutoka katika jamii husika wanazoishi kisha serikali itawapa mafunzo ya miezi sita wahudumu hao ili waweze kupata maarifa na ujuzi zaidi katika maeneo mbalimbali ikiwemo masuala ya Kifua Kikuu, VVU/UKIMWI, Malaria na Lishe, Water and Sanitation, Malezi na Makuzi ya Mtoto, miezi mitatu watakua darasani na miezi mitatu mingine watakua field ili kuhakikisha wanakua na ujuzi unaotakiwa" Ameeleza.

 Bi Somoe Ngaokola ni mtoa huduma kwa jamii chini ya Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka MSF linalotoa huduma za afya ya Mama na Mtoto katika kituo cha afya cha Liwale Mji anaeleza namna ambavyo anatoa elimu juu ya huduma za afya hususani kwa wamama wajawazito, malezi ya watoto na elimu mtambuka.

"Kupitia MSF tumewezeshwa kwa kupata mafunzo ambayo yametuwezesha kuwahudumia wanajamii wenzetu katika masuala mbalimbali hususani kuelimisha na kuwashawishi wanawake kuhudhuria kliniki wanaposhika ujauzito lakini pia elimu ya unyonyeshaji wa watoto haswa umuhimu wa kunyonyesha mtoto miezi sita bila ya kumpatia kitu kingine chochote kama vile maji, dalili za hatari kwa mtoto kama degedege na dalili za hatari kwa mama baada ya kujifungua kama vile kuvimba miguu na mwili kubadilika rangi wasikimbilie kwa waganga wa kienyeji waje hospitali kupata huduma kwa maana hizo ni dalili za kifafa cha mimba hawajarogwa pamoja na elimu nyinginezo mtambuka ikiwemo usafi"

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.