• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

SERIKALI YAZINDUA AWAMU YA TATU YA MRADI WA TIMIZA ILI KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KWA VIJANA WA UMRI BALEHE

Posted on: February 20th, 2025

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Ummy Nderiananga, kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amezindua awamu ya tatu ya mradi wa Timiza Malengo 2024-2026 unaotarajiwa kutekelezwa katika Mikoa 10 na Halmashauri 36 nchini. 


Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mhe. Ummy amesema kuwa mradi wa Timiza Malengo unalenga kupunguza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) kwa vijana balehe wenye umri wa kati ya miaka 18 hadi 24 walio mashuleni na nje ya mfumo wa elimu kwa kuwajengea uwezo wa kujikinga dhidi ya maambukizi na kuwawezesha kiuchumi katika Mikoa ya Singida, Lindi, Morogoro, Njombe, Dodoma, Tabora, Tanga, Ruvuma, Geita na Mara.


Aidha, Mhe. Ummy ameeleza kuwa serikali inaendelea na mipango ya kisera na kimuundo kuhakikisha hadi ufikapo 2030 Tanzania iwe imefanikiwa kufikia 03 katika mapambano dhidi ya maambukizi mapya, kuzuia vifo vitokanavyo na VVU/UKIMWI pamoja na unyanyapaa na ubaguzi kwa watu wanaoishi na maambukizi.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dkt. Catherine Joachim, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutekeleza mradi huo, akibainisha kuwa itawafikia vijana balehe walio katika hatari zaidi ya kupata maambukizi ya VVU na kusaidia kupunguza kasi ya maambukizi nchini.


Pia, Dkt. Catherine ameeleza kuwa mradi utasaidia kufikia malengo ya kitaifa, kikanda na kimataifa katika mapambano dhidi ya UKIMWI ifikapo 2030, kuongeza wigo wa utekelezaji wa afua za kinga kwa vijana, kutunisha mfuko wa udhamini pamoja na kuboresha mifumo ya uratibu.


Aidha, mradi wa Timiza Malengo kwa awamu ya tatu umelenga kuwafikia na vijana balehe wa kiume na kuwapa mafunzo stadi, kuwaunganisha na taasisi za ufundi hususan VETA, pamoja na kuwaunganisha na taasisi za kifedha zinazotoa mikopo nafuu ikiwemo mikopo ya 10% inayoratibiwa na serikali kupitia wizara ya TAMISEMI.


Sambamba na uzinduzi wa mradi wa Timiza Malengo, Mhe. Ummy amezindua kampeni ya Tusonge na Samia Kutokomeza UKIMWI, ambayo inalenga kuhamasisha utekelezaji wa afua mbalimbali za kudhibiti VVU na UKIMWI nchini, kampeni hii inatarajiwa kuongeza mwamko wa jamii kuhusu hatua madhubuti za kujikinga na kusaidia katika kufanikisha lengo la kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.