• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

UJENZI WA SHULE YA MSINGI LIKONG’O WENYE THAMANI YA BIL 1.2 UMEFIKA 53% DC LINDI APONGEZA

Posted on: October 2nd, 2025

Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) kwa kushirikiana na Equinor na Shell ambao ni wawekezaji wa mradi wa uzalishaji na usindikaji wa Gesi Asilia Tanzania (TLNG) wameendeleza ujenzi wa shule ya msingi Likongo unaogharimu kiasi cha Bilioni 1.2.

Akizungumza mara baada ya kutembelea majengo ya shule hiyo Mhandisi Burhan Omary amesema kuwa mradi huo wa shule ya msingi Likongo utagharimu zaidi ya Bilioni 1.2 ambao unatarajiwa kukamilika Desemba 27, 2025 ambapo hafi sasa umefikia 53%.

Mhandisi Omary ameendelea kusema kuwa ujenzi wa shule hiyo utakuwa na madarasa 9,na madarasa mawili ya shule ya awali nyumba za walimu pamoja na jengo la utawala.

"Mradi huu utakapo malizika utagharimu zaidi ya Sh.1.2 Bilioni na hadi sasa tumeweza kuajiri wafanyakazi wazawa wapatao 107, pia ujenzi wa shule hii ukikamilika

utakuwa umemaliza changamoto ya elimu katıka eneo hili kwani walimu watakuwa wanaishi hapa hapa shuleni, kuliko ilivyosasa walimu wanatoka mbali kuja kufundisha hapa Likongo."amesema Mhandisi Omary.

Naye Ofisa maendeleo mwandamizi kutoka TPDC Ally Mluge amesema kuwa lengo la TPDC ni kutoa ushirikiano kwa serikali na kurudisha kwa jamii kama kuboresha miundombinu mbalimbali ikiwemo shule .

"Tumekuwa na kawaida ya kurudisha kwa jamii katika kuboresha miundombinu mbalimbali kama shule na kutoa ushirikiano kwa serikali katika kuleta maendeleo. "amesema Mluge.

Mwenyekiti Renatus Nyanda akiongozana na kamati ya CSR amesema kuwa ujenzi wa mradi wa shule ni mradi wa mfano kwani utachochea ukuaji wa elimu katika eneo la Likong’o.

"Niwahakikishie wananchi wa Likong’o kuwa ifikapo 2026 watoto wenu wataanza kusoma katika shule hii mpya, napia niwapongeze sana wasimamizi wa mradi, csr tumelidhishwa na maendeleo ya mradi huu." amesema Nyanda.

Mkuu wa Wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva amewashukuru na kuwapongeza TPDC kwa kuweza kuboresha mazingira ya elimu pamoja na kuinua hadhi ya shule.

"Tunawashukuru sana TPDC kwa kuweza kurudisha kwa jamii na kutuboresha mazingira ya shule yetu imani yangu kwenu mradi utakamilika kwa wakati na ifikapo 2026 wanafunzi wa darasa la awali wataanza kuyatumia madarasa yao."amesema Mwanziva.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • RAS LINDI SPORTS CLUB YAKABIDHI KOMBE LA SHIMIWI KWA RAS.

    October 10, 2025
  • ICU YA ZAIDI YA MIL 600 YASHUSHWA NACHINGWEA.

    October 09, 2025
  • MRADI WA HEWA TIBA HALMASHAURI YA RUANGWA

    October 09, 2025
  • MAFANIKIO YA AWAMU YA SITA

    October 10, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.