• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

W

Posted on: September 27th, 2017

Wananchi watakiwa kutumia fursa ya uwepo wa madaktari bingwa kupima afya zao.

Wananchi wa Mkoa wa Lindi watakiwa kutumia vizuri fursa ya uwepo wa madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupima afya zao na kupatiwa matibabu.

Haya yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi wakati akizindua utoaji huduma za vipimo na matibabu unaofanywa na madaktari bingwa wakishirikiana na madaktari na wataalam katika hospitali ya rufaa ya sokoine, huduma ambayo inatolewa kuanzia tar. 25-30/09/2017.

Uzinduzi huu ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali ambao ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya, Mhe. Anna Makinda (Spika Mstaafu), Katibu Tawala Mkoa wa Lindi, Ndg. Ramadhani Kaswa, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Ndg. Aifena Mramba, Wah. Wakuu wa Wilaya na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Lindi, Ndg. Mohamed Lihumbo, Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Lindi, wataalam wa NHIF, Sekretarieti ya Mkoa, hospitali ya rufaa ya sokoine na wananchi waliokuwa wamekuja kupata huduma.

Madaktari hawa bingwa wameletwa chini ya ufadhili wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa ambao pia wameleta vifaa tiba pamoja na madawa. Huduma zitakazotolewa ni pamoja na za magonjwa ya moyo, magonjwa ya ndani, magonjwa ya mfumo wa mkojo, magonjwa ya akina mama – kike na uzazi, magonjwa ya macho, sikio, pua na koo na magonjwa mahututi na usingizi.

Mhe. Zambi aliwaeleza wananchi waliokuwa wamefika kupata matibabu kutumia fursa hii vizuri na kuhakikisha wanawajulisha ndugu zao wenye matatizo mbalimbali ya kiafya. Ambapo pia amevisihi vyombo vya habari kuwatangazia wananchi juu ya uwepo wa madaktari hawa.

“Nimshukuru Mhe. Makinda na uongozi mzima wa NHIF kwa kufanikisha zoezi hili la upimaji afya na utoaji matibabu kunakofanywa na madaktari bingwa kwani hii inasaidia sana katika kusogeza huduma kwa wananchi wa chini ikiwa ni pamoja na kuwapunguzia gharama katika kupata huduma”, alisema Mhe. Zambi.

Aidha, madaktari na watumishi wa hospitali ya rufaa ya sokoine wametakiwa kutumia fursa hii ya uwepo wa madaktari bingwa kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu utoaji huduma za afya ili wakiondoka waweze kuendelea kutoa baadhi ya huduma. Pia amemuagiza mganga mkuu wa mkoa kuvitunza vifaa vyote vitakavyoachwa na NHIF na kuhakikisha vinatoa huduma kwa wananchi.

Vilevile, Mhe. Zambi amemuagiza Katibu Tawala Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri, Mganga Mkuu wa Mkoa na Waganga Wakuu katika Halmashauri kuhakikisha wanatumia vizuri fursa ya mikopo inayotolewa na NHIF ya kuboresha huduma za afya ili kuimarisha utoaji huduma katika vituo.

Kabla ya uzinduzi kufanyika, Mhe. Makinda alielezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na NHIF ikiwa ni pamoja na utoaji mikopo inayosaidia katika kuboresha huduma za afya. Pia aliwasihi wananchi kujiunga na bima ya afya kwani ugonjwa hutokea muda wowote. Aidha, Mhe. Makinda aliwataka watumishi wa afya kubadilika kwani kumekuwepo na malalamiko kwa baadhi ya watumishi wa afya kutumia lugha mbaya na kutowajali wagonjwa.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.