• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufuatiliaji na Tathmini
      • Maendeleo ya Jamii
      • Government Communication
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WADAU WA MAENDELEO YA JAMII LINDI WAKUTANA KUJADILI MPANGO MKAKATI WA KUPINGA UKATILI KWA WANAWAKE NA WATOTO

Posted on: November 26th, 2025

WADAU WA MAENDELEO YA JAMII LINDI WAKUTANA KUJADILI MPANGO MKAKATI WA KUPINGA UKATILI KWA WANAWAKE NA WATOTO.


Mkoa wa Lindi umefanya kikao na wadau mbalimbali wa Maendeleo ya Jamii wakiwemo wadau kutoka serikalini, asasi za kiraia na taasisi za dini kwa lengo la kupitia rasimu ya Mpango Mkakati wa Kupinga Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto kwa kipindi cha miaka mitano ijayo (2025/26- 2029/30).


Ndugu. Charles Kigahe, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Lindi ameeleza kuwa Rasimu hiyo imejikita katika kuimarisha ulinzi, ustawi na fursa kwa wanawake na watoto kwa kuelekeza nguvu kubwa katika kuboresha haki za binadamu, huduma muhimu za kijamii, uwezeshaji kiuchumi na kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi mbalimbali za maamuzi.


Katika majadiliano hayo, wadau walisisitiza umuhimu wa kuimarisha masuala ya haki za binadamu kwa kuhakikisha wanawake na watoto wanapata hifadhi, usawa na msaada pale wanapokumbana na vitendo vya ukatili kwa kuboresha huduma za ustawi wa jamii zikiwemo huduma za msaada wa kisheria, usaidizi wa kisaikolojia, ulinzi wa mtoto na mifumo rafiki ya utoaji taarifa za ukatili.


Aidha, uwezeshaji wa wanawake kiuchumi kupitia mafunzo, mitaji midogo, ajira na programu za kuinua uchumi wa kaya zinatarajiwa kupunguza utegemezi unaowafanya wanawake wengi kuwa katika hatari ya kunyanyaswa na kukosa uhuru wa maamuzi.


Wadau pia walijadili kwa kina changamoto ya mdondoko wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari unaochangiwa na mila na desturi zisizofaa kama Jando na Unyago hususan inapotekelezwa bila kuzingatia haki na ustawi wa watoto, pamoja na changamoto ya kukosekana kwa chakula shuleni ambayo husababisha wanafunzi wengi kukatisha masomo na kupendekeza mikakati madhubuti ya kuelimisha jamii, kuimarisha huduma shuleni na kuweka mifumo ya ufuatiliaji ili kuhakikisha watoto wanasalia shuleni na kumaliza masomo.


Mpango mkakati huu unatarajiwa kuwa nyenzo muhimu katika kupunguza ukatili, kuimarisha ustawi wa wanawake na watoto, na kupandisha kiwango cha elimu katika Mkoa wa Lindi kwa miaka ijayo.





Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI, TAASISI ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI ZATAKIWA KUIMARISHA HUDUMA KWA WAJASIRIAMALI MKOANI LINDI

    November 27, 2025
  • UJENZI WA MADARAJA NA BARABARA KUSINI WAFIKIA 88%

    November 27, 2025
  • DKT. SHEKALAGHE AAGIZA HUDUMA KUANZA KUTOLEWA HOSPITALI MPYA YA RUFAA LINDI SOKOINE IFIKAPO JANUARI 1, 2026

    November 26, 2025
  • BODI YA KOROSHO TANZANIA YAWAPIGA MSASA MAAFISA BIASHARA MKOA WA LINDI.

    November 26, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.