• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wadau watakiwa kuusimamia Mpango Mkakati wa Elimu 2020

Posted on: February 8th, 2020

 Wadau watakiwa kuusimami Mpango Mkakati wa Elimu 2020

Wadau wa elimu mkoa wa Lindi watakiwa kukuusimamia mpango mkakati wa elimu 2020 ili kuondokana na ufaulu usioridhisha.

Wadau hao wakiwemo Viongozi mbalimbali wa serikali na taasisi zisizo za kiserikali, walimu, wazazi na wanafunzi walikutana katika Uwanja wa Ilulu wakati wa sherehe fupi za uzinduzi wa mpango mkakati wa elimu mkoa wa Lindi mwaka 2020 pamoja na utoaji tuzo kwa waliofanya vizuri katika mitihani mbalimbali ya taifa kwa mwaka 2019.

Akizungumza kabla ya kuuzindua mpango mkakati huo, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi alisema kwamba mkoa umekuwa ukiweka mikakati mbalimbali ambayo pia ilishirikishwa kwa viongozi na jamii katika ngazi zote kitu ambacho kimesaidia mkoa kuongeza ufaulu katika mitihani mbalimbali ya kitaifa ya mwaka 2020.

“Mpango Mkakati huu ninaouzindua leo ndiyo dira yetu katika kuondokana na ufaulu usioridhisha kwa watoto wetu kwani mambo ya msingi ambayo yamekuwa ni changamoto katika utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 yamebainishwa”, alisema Mhe. Zambi.

Mkuu wa Mkoa Zambi alisema kuwa Mpango Mkakati huo umegusa mambo yafuatayo ambayo yatahitaji usimamizi na ufuatiliaji:-

  1. Kupunguza au kuondoa tatizo la utoro kwa wanafunzi.
  2. Kukomesha tatizo la wanafunzi wa kike wanaopewa ujauzito.
  3. Kusimamia utoaji wa chakula kwa wanafunzi shuleni.
  4. Walimu kukamilisha mada zao mapema.
  5. Kusimamia na kuendesha Vituo vya za Mada ngumu.
  6. Utendaji usioridhisha kwa baadhi ya viongozi wa Elimu na Walimu
  7. Usimamizi na ufuatiliaji wa ujifunzaji shuleni
  8. Moyo wa kujituma na kujitolea katika kazi na,
  9. Utoaji wa Tuzo

Hivyo amewataka wadau wote kushirikiana katika kuhakikisha mpango mkakati huo unatekelezwa kikamilifu kwa kila mmoja kufanya ufuatiliaji katika eneo lake.

Mkuu wa mkoa Zambi pia amewapongeza wote waliopata tuzo mbalimbali kama motisha kwa kufanya kazi nzuri na kuwataka kuendeleza bidii hiyo ili mkoa uweze kufanya vizuri zaidi. Aidha, amewasihi wale ambao hawakufanya vizuri kuhakikisha wanabadilika ili kuweze kufikia malengo ambayo yamewekwa na mkoa.

Naye Afisa Elimu Mkoa wa Lindi, Vicent Kayombo alisema katika mtihani wa taifa wa kidato cha sita mkoa umekuwa wa kwanza kati ya mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani, tena kwa kutokuwa na daraja sifuri. Kwa kidato cha nne mkoa umeshika nafasi ya 23 kati ya mikoa 31 Tanzania Bara na Visiwani ambapo asilimia ya ufaulu imepanda kutoka 69.3 ya mwaka 2018 mpaka asilimia 83.2. Kwa upande wa kidato cha pili mkoa haukufanya vizuri kwani umeshika nafasi ya 26 kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Katika mtihani wa kitaifa wa darasa la saba mwaka 2019 mkoa umeshika nafasi ya 18 kutoka nafasi ya 24 mwaka 2018, ambapo ufaulu umepanda kutoka asilimia 68.71 mwaka 2018 hadi asilimia 76.48 mwaka 2019. Kwa darasa la nne mkoa umeshika nafasi ya 10 kitaifa kutoka nafasi ya 20 mwaka 2018, ambapo ufaulu umefikia asilimia 94.7 kutoka 91.96 mwaka 2018.

Kwa upande wa walimu ambao shule zao au walimu wao wamepata tuzo, wameupongeza uongozi wa mkoa kwa kuamua kuandaa sherehe hizo ambazo zimewafanya walimu kutoka maeneo mbalimbali ndani ya mkoa kuweza kukutana na kupongezana kwa pamoja. Aidha, wameahidi kurudi kuendelea na kazi wakiwa na nguvu mpya na kwamba wapo tayari kupambana kuhakikisha mkoa unaendelea kunyanyuka kiufaulu.

Sherehe hizi za utoaji tuzo zitakuwa zikifanyika kila mwaka ambapo wale waliofanya vizuri watapewa tuzo na fedha kama motisha na kwa wale watakao kuwa wamefanya vibaya kupatiwa bendera nyeuzi ambazo zitatakiwa kusimamishwa ndani ya ofisi zao lengo likiwa ni kuwakumbusha juu ya matokeo mabovu waliyoyapata na kwamba wanahitaji kuongeza jitihada.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.