• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WAHITIMU WA MAFUNZO YA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII WAPATIWA VYETI NA VITENDEA KAZI

Posted on: September 8th, 2025


- "CHW, Nyumba kwa Nyumba, Hatuachi Mtu"

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa OR-TAMISEMI kwa kushirikiana na Wadau wa Sekta ya Afya imekabidhi seti ya vitendea kazi kwa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHW) 3,561 waliohitimu mafunzo ya kutoa huduma za afya ngazi jamii.


Katika hafla ya kukabidhi vyeti na vitendea kazi kwa wahitimu 222 wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, wakiwakilisha kundi la Wahudumu 3,561 wa awamu ya kwanza ya wahudumu waliohitimu mafunzo hayo katika mikoa 12, Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Omary amewataka wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii WAJA kuzingatia miongozo, taratibu,maadili na tahadhari zote walizoelekezwa kipindi cha mafunzo wanapokwenda kutoa huduma katika jamii zao ili kufikia lengo la mpango wa serikali wa kuongeza nguvu kazi na kuwasogezea wananchi huduma za afya msingi na matibabu ya awali.


Aidha, Bi. Zuwena amesema Serikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa huduma za afya karibu zaidi na wananchi na wahudumu wa afya ngazi ya jamii wamehitimu na wapo tayari kwa ajili ya kuanza kazi wakiwa na nyenzo zote muhimu kwa ajili ya kufanya kazi kwa ufanisi.


“Mpango huu ulizinduliwa mwaka 2024 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Phillip Isdor Mpango, hapo nyuma katika miaka 1970 tulikuwa na mpango huu pia lakini ulipitia changamoto za uratibu na awamu hii programu hii ya WAJA imeboreshwa zaidi ili kuleta tija zaidi katika kuimarisha huduma za kinga ndani ya jamii ili kufikia lengo la Huduma za Afya kwa wote ifikapo mwaka 2030,” amesema Bi. Zuwena.


Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Kheri Kagya amesema ni matarajio ya serikali kuwa uwepo wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii utasaidia utolewaji wa huduma za afya, Uzazi na mtoto, Lishe, Usafi wa mazingira na magonjwa ya mlipuko pamoja na kuwa kiunganishi muhimu baina ya jamii na vituo vya kutolea huduma za afya.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI WA DKT. SAMIA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA BOBEZI KATIKA HOSPITALI 7 ZA WILAYA, MKOANI LINDI.

    September 15, 2025
  • KAMBI YA MADAKTARI BINGWA NA BINGWA BOBEZI AWAMU YA NNE YAANZA KAZI MKOANI LINDI

    September 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA NA BOBEZI 49 WA MAMA SAMIA WAPOKELEWA LINDI.

    September 15, 2025
  • RAS LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA KUPITIA NA KUJADILI AFUA ZA LISHE APRIL- JUNI 2025.

    September 13, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.