• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WANANCHI WA MILOLA WAISHUKURU SERIKALI KWA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA.

Posted on: March 3rd, 2023

Wananchi wa Kijiji cha Milola, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi wameishukuru serikali kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa kujengewa daraja ambalo limekuwa kiunganishi na kichochezi cha mahusiano mazuri yaliyopo kati yao na wananchi wengine waishio maeneo ya jirani ikiwemo Nangaru na Kikomolela.

Hayo yamesemwa wakati wa ziara ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bwana Ngusa Samike yenye lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya Barabara inayotekelezwa na kusimamiwa na TARURA katika mkoa wa Lindi.

Awali akitoa maelezo ya mradi huo Meneja wa TARURA wilaya ya Lindi Mhandisi Dawson Paschal amesema “ ujenzi wa daraja la Milola umegharimu kiasi cha Milioni 300 ambapo ulihusisha ujenzi wa daraja kwa na ujenzi wa vented drift katika barabara ya Milola- Nangaru, mradi huu umetekelezwa na Mkandarasi M/s Construction Company Limited ambapo mkataba wake ulianza tarehe 8 Agosti na kukamilika tarehe 8 Disemba 2022 na utekelezaji wake umekamilika kwa asilimia 100’’

Selemani Yusuph Namtumba,Mkazi wa Milola ameeleza shukrani zake kwa serikali kwa ujenzi wa daraja la Milola na ukarabati wa barabara unaoendelea “ Tunashukuru sana kwa ujenzi huu unaoendelea hasa kwa barabara hii ya Milola-Nangaru kwa maana ilikua ni kikwazo kidogo kwa shughuli zetu tunazozifanya kila siku lakini kwa sasa tuna matumaini makubwa mno, kabla ya ujenzi huu hali ya usafiri ilikua ni mbaya mno hatukuweza kupita eneo lile hata kwa baiskeri lakini sasa tunapita na usafiri wowote ule hii imefanya kuimarika hata kwa ufanyaji wetu wa baishara na usafirishaji wa bidhaa zetu kwa ujumla”

Naye, Karim Mmaka ameipongeza TARURA kwa kazi wanazozifanya hasa ujenzi wa barabara na daraja katika maeneo ya Milola na kuongeza kuwa ujenzi huo unaenda kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa katika maeneo yao “ Nipende kuchukua nafasi hii kuipongeza tu TARURA na serikali kwa ujumla kwa kazi kubwa wanayoifanya, daraja hili linaenda kupunguza njia ya mzunguko tuliyokuwa tunapita mwanzo kutoka hapa Milola ili tuweze kufika sehemu tuliyokuwa tunakusudia Kwenda, hili daraja limekuwa mkombozi kwetu kwasababu linaenda kupunguza vifo vya watu hasa wanafunzi wanaotoka ng’ambo ya pili kuja huku kuja shuleni katika majira ya masika”

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.