• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

WANANCHI WATAKIWA KULINDA MRADI WA MAJI

Posted on: September 26th, 2017

WANANCHI WATAKIWA KULINDA MRADI WA MAJI

Wananchi wa Mtaa wa Jangwani Kata ya Chinkonji katika Manispaa ya Lindi, wametakiwa kuusimamia na kulinda mradi wa maji.

Mradi huu maji wa Chikonji ambao una awamu tatu ambapo awamu ya kwanza ni ujenzi wa miundombinu ya vyanzo pamoja na ile ya usambaza maji Chikonji Kusini na Kaskazini kwa gharama ya shilingi 1,171,919,650. Awamu ya pili ni ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa maji Jangwani na Nanyanje kwa gharama ya shilingi 315,261,408. Awamu ya tatu ni ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa maji Mtaa wa Mkanga kwa gharama ya shilingi 483,720,490, hivyo jumla ya fedha za mradi mzima ni shilingi 1,970,901,548.

Haya aliyasema Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kata ya Chikonji ambapo katika Mtaa wa Jangwani alikagua shule ya msingi Jangwani na kufanya mkutano na wananchi wa Jangwani.

Mhe. Zambi alilazimika kuyasema haya baada ya kupata malalamiko toka kwa mhandisi wa maji kuwa wananchi wamekuwa na tabia ya kukata mabomba na kudumbukiza vitu ili kukwamisha mradi usikamilike wakati wanayoshida kubwa ya maji.

“Wananchi mradi huu wa maji ni wenu, hivyo mnao wajibu mkubwa sana wa kuulinda. Serikali inajenga mradi na ukishakamilika inaukabidhi kwenu ili muuendeshe kupitia kamati yenu ya maji ambayo wajumbe wake mnawachagua wenyewe”, aliesema Mhe. Zambi.

Katika mkutano wa hadhara, alipata lalamiko la ubovu wa barabara ambapo alimuagiza Meneja wa TARURA kuhakikisha anaingiza barabara ya Muhimbili-Jangwani na Jangwani-Chikonji kwenye mpango wa bajeti ya mwaka 2018/2019 lakini halmashauri iangalie kama itapata fedha zozote itengeneze barabara hizi.

Pia alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha katika bajeti ya 2018/2019 wanaingiza ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu katika shule ya msingi Jangwani. Aidha, Mhe. Zambi aliagiza choo cha walimu cha kudumu kijengwa na kukamilika ifikapo Decemba, 2017.

Baada ya kumaliza kuongea na wananchi wa Mtaa wa Jangwani, Mhe. Zambi alitembelea mradi wa umwagiliaji kwa njia ya matone – Mingoyo ambapo alimtaka kuhakikisha anawapelekea mbegu wanakikundi ili shughuli za kilimo zeweze kuanza.

Aidha, alifanya mkutano wa hadhara katika Kata ya Nachingwea ambapo alisikiliza kero mbalimbali za wananchi huku kero kubwa ikiwa ni utaratibu mbovu wa ugawaji wa viwanja vilivyopo Mtaa wa Mlandege.

Mhe. Zambi baada ya kusikiliza maelezo kutoka pande zote za viongozi wa Kata na wanachi, alibaini kuwa kulikuwa na mapungufu katika ugawaji wa viwanja na kumuagiza Katibu Tawala Wilaya ya Lindi, Ndg. Thomas Safari ambaye pia alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Lindi kuhakikisha anaunda tume itakayofanya kazi kwa mwezi mmoja kupitia upya taratibu zilizotumika kugawa viwanja.

Aidha, aliagiza kuwa wale wote waliopewa viwanja ambao hawajajenga wasijenge kwani inaonekana wazi kuwa wapo wananchi waliostahili kupewa maeneo hayo na hawajapewa badala yake wanatafutiwa eneo jingine.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • MHE. TELACK AZINDUA MPANGO MKAKATI WA ELIMU MKOA WA LINDI KWA MWAKA 2025

    May 02, 2025
  • RC TELACK AKABIDHI TUZO ZA ELIMU KWA WALIMU,WANAFUNZI NA HALMASHAURI ZILIZOFANYA VIZURI MKOANI LINDI.

    May 02, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.