• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Lindi Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Lindi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Menejimenti ya Serikali za Mtaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Kilwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Lindi
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Liwale
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Nachingwea
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
    • Ruangwa
      • Historia ya Wilaya
      • Uongozi wa Wilaya
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
    • Halmashauri ya Manispaa ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Liwale
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Jarida
    • Fomu
    • Sheria
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Watanzania watakiwa kutunza na kulinda tamaduni zao

Posted on: October 28th, 2018

Watanzania watakiwa kutunza na kulinda tamaduni zao

Mhe. Kassim Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani amewataka watanzania kutunza na kulinda tamaduni zao kwa maendeleo ya taifa.

Haya aliyasema alipotembelea tamasha la utamaduni wa watu wa mkoa wa Lindi lililofanyika katika kijiji cha makumbusho ya taifa mkoani Dar es Salaam kuanzia tarehe 25-28/10/2018. Katika tamasha hili wanalindi walipata fursa ya kuonyesha mambo mbalimbali yanayohusu tamaduni zao mfano, ngoma, vyakula, vifaa vya jadi, nyumba zao, ikiwa ni pamoja na uwasilishaji wa mada mbalimbali zinazohusu tamaduni na maendeleo ya mkoa kwa ujumla.

Mhe. Majaliwa alisema kuwa kupitia matamasha kama haya watanzani wanapata fusa ya kujifunza tamaduni za watu wa mikoa mingine na hii inasaidia kuendelea kuwafanya watanzania kuwa na mshikamano. Pia aliwasihi wanalindi kuhakikisha wanalitumia vizuri tamasha hilo kwa kuonyesha tamaduni zao na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo katika mkoa ili wawekezaji waweze kuja kuwekeza.

“Serikali itaendelea kulinda na kutunza tamaduni za watanzania kwa maendeleo ya taifa”, alisema Mhe. Majaliwa. “Serikali inatambua umuhimu wa tamaduni zetu katika kusimamia maadili ya watanzani na hivyo kusaidia kuwa na taifa la wananchi wenye maadili hasa kwa kundi la vijana ambalo kwa sasa limeonekana kuporomoka kimaadili”, aliongeza Mhe. Majaliwa.

Aidha, amewapongeza wanalindi kwa kujitokeza kwa wingi kuja kushiriki katika tamasha na ameipongeza kamati kwa ujumla ikiongozwa na Mhe. Godfrey Zambi, Mkuu wa Mkoa wa Lindi kwa kazi kubwa na nzuri ya maandalizi waliyoifanya.

Pia aliuagiza mkoa kwa kushirikiana na kijiji cha makumbusho kuangalia uwezekano wa tamasha hili liwe linafanyika kila mwaka tarehe 25-28 October. Vilevile mkoa umeagizwa kutafuta eneo ambalo litakuwa ni katikati kwa wilaya zote na kuanza taratibu za ujenzi wa makumbusho katika mkoa ambapo vitu mbalimbali vya tamaduni za watu wa mkoa wa Lindi zitaonyeshwa na matamasha ya utamaduni ndani ya mkoa yatakuwa yakifanyika hapo.

Naye Mhe. Zambi alimshukuri Waziri Mkuu kwa kuja kutembelea tamasha na kujionea mambo mbalimbali ya tamaduni za watu wa Lindi ambapo pia alimuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote aliyoyatoa. Pia aliwapongeza makumbusho ya taifa kwa ushirikiano mkubwa walioutoa wakati wa maandalizi ya tamasha hili pamoja na kamati ya maandalizi.

Mkurugenzi wa kijiji cha makumbusho, Bi. Agnes Pinda alisema kuwa katika tamasha hili wanajamii wa mkoa wa Lindi wameshiriki vuzuri sana kwa kuonyesha mambo mbalimbali ya tamaduni zao. Vilevile wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam nao wamefika kwa wingi ikiwa ni pamoja na wageni kutoka nje ya nchi. Ni waombe wanalindi kuendelea kujitoa na kujitokeza kwa wingi pindi matamasha kama haya yanapoandaliwa.

Mmoja wa washiriki wa tamasha hili Bw. Kindamba amesema tamasha hili ni zuri sana kwani limewakutanisha wasaniii mbalimbali wa ngoma, na sanaa nyingine ambapo wanapata fursa ya kujifunza mambo mengine kupitia wenzao.

Aidha, Mhe. Majaliwa aliwapa salam za Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania washiriki wa tamasha na kuwaeleza kuwa anawapongeza wanalindi kwa kufanikisha tamasha hili.

Mhe. Majaliwa pia aliwaeleza kuwa kwa sasa serikali imesitisha minada ya korosho kutokana na kushuka kwa bei ili iweze kufanya tathmini ya kina na kutafuta ufumbuzi wa soko hilo. Hivyo amewasihi wakulima wa korosho kuwa watulivu katika kipindi hiki ambachoserikali inalifanyia kazi suala hili.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALI0CHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021-MKOA WA LINDI March 29, 2021
  • Vitabu vya kalenda za utekelezaji wa mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari February 08, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO KWA MKOA WA LINDI 2022 May 09, 2022
  • FOMU ZA MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI KWA MKOA WA LINDI (JOINING INSTRUCTIONS) December 16, 2020
  • tazama zote

Habari Mpya

  • VIJIJI VYOTE 523 LINDI VYAPATA UMEME

    May 06, 2025
  • UJENZI WA UDSM TAWI LA LINDI WAFIKIA 45%, RC TELACK APONGEZA NA KUSISITIZA KASI NA UBORA WA UJENZI

    May 05, 2025
  • JAMII NA WAZAZI WATAKIA KURUDI KUBEBA JUKUMU LA MALEZI KWA WATOTO

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA WA LINDI AONGOZA KIKAO CHA LISHE NGAZI YA MKOA

    May 03, 2025
  • tazama zote

Video

CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO YA CHAMA CHAO MAPEMA ILI KUWAPA UTULIVU WANACHAMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal
  • Kilwa District Council
  • Nachingwea Disctrict Council
  • Ruangwa District Council
  • Liwale District Council
  • Lindi Municipal
  • Lindi District Council

Kurasa mashuhuri

  • Public Procurement Reguratory Authority
  • Tamisemi
  • e-Government Agency
  • Watumishi Portal
  • Sekretarieti ya ajira
  • CWT WASHAURIWA KUMALIZA MIGOGORO ILI WANACHAMA WAPATE UTULIVU

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi

    Sanduku la Posta: P.o Box 1054 Lindi

    Simu: 023-220-2098

    Rununu:

    Barua pepe: ras.lindi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hati miliki ©2017 Lindi . Haki zote zimehifadhiwa.